-
Herode Mkuu—Mjenzi StadiAmkeni!—2009 | Septemba
-
-
Majumba ya Kifalme ya Kifahari
Hata hivyo, Herode alikuwa na majumba mengine ya kifalme aliyoyatumia katika majira ya baridi kali. Alijenga ngome kwenye mwamba tambarare ulioinuka zaidi ya mita 400 juu ya Bahari ya Chumvi unaoitwa Masada. Katika eneo hilo, alijenga jumba la kifalme lenye orofa tatu lililokuwa na veranda na vidimbwi vya kuogea, na pia jumba lingine la kifalme lililokuwa na bafu zenye mabomba ya kupasha maji moto na choo cha kuvuta maji!
Katika eneo hilo la jangwani, Herode alijenga mahali ambapo angestarehe na kuboresha afya yake. Alijenga visima 12 ambavyo vingeweza kubeba lita milioni 40 hivi za maji. Kwa kuwa ngome hiyo pia ilikuwa mfumo mzuri wa kukusanya na kuhifadhi maji ya mvua, kulikuwa na maji ya kutosha kwa ajili ya kilimo, kuoga, na kuogelea.
-
-
Herode Mkuu—Mjenzi StadiAmkeni!—2009 | Septemba
-
-
[Picha katika ukurasa wa 26]
MASADA
Magofu ya kasri lenye orofa tatu
[Hisani]
Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.
-