-
Nifanye Nini Ili Niache Kufikiria Ngono Saa Zote?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
Tatizo la Kupiga Punyeto
Vijana fulani hujaribu kupunguza tamaa ya ngono kwa kupiga punyeto. Lakini kufanya hivyo kunaweza kutokeza matatizo makubwa. Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye madhara, na kutamani.” (Wakolosai 3:5) Kupiga punyeto ni kinyume kabisa cha ‘kuua hamu ya ngono.’ Kwa kweli, kupiga punyeto huchochea na kukuza hamu hiyo!
Kupiga punyeto kwaweza kukufanya kuwa mtumwa wa tamaa zako. (Tito 3:3) Hatua moja unayoweza kuchukua ili kushinda zoea hilo ni kuzungumza na mtu unayemtumaini. Mkristo aliyekuwa na tatizo la kupiga punyeto kwa miaka mingi anasema hivi: “Laiti ningeweza kupata ujasiri wa kuzungumza na mtu fulani kuhusu tatizo hilo nilipokuwa kijana! Kwa miaka mingi nilisumbuliwa na hisia za hatia, nazo ziliathiri sana uhusiano wangu na wengine, na zaidi ya yote, uhusiano wangu na Yehova.”
Ni nani unayeweza kuongea naye? Mara nyingi ingefaa kuzungumza na mzazi. Au huenda Mkristo mkomavu kutanikoni anaweza kukusaidia. Unaweza kuanza kwa kusema, “Ningependa kuzungumza nawe kuhusu tatizo linalonisumbua sana.”
André aliongea na mzee Mkristo, naye anafurahi kwamba alifanya hivyo. “Mzee huyo alipokuwa akinisikiliza, alilengwa-lengwa na machozi,” André anasema. “Nilipomaliza kuzungumza, alinihakikishia kwamba Yehova ananipenda. Aliniambia kwamba watu wengi wana tatizo kama langu. Aliahidi kwamba atakuwa akizungumza nami mara kwa mara kuona nimefanya maendeleo kiasi gani na kuniletea habari zaidi kutoka katika vitabu vinavyotegemea Biblia. Baada ya kuongea naye, niliazimia kupiga vita zoea hilo—hata ikiwa ningeanguka mara moja moja.”
Mário aliamua kuongea na baba yake, aliyemjali sana na kuelewa hali yake. Hata alikiri mbele za Mário kwamba alipokuwa kijana haikuwa rahisi kwake kushinda zoea hilo. “Nilitiwa moyo sana na mazungumzo hayo ya waziwazi na unyoofu wa baba yangu,” asema Mário. “Nilijiambia, ikiwa alifaulu, hata mimi nitafaulu. Niliguswa moyo sana na mtazamo wa baba yangu hivi kwamba sikujizuia kulia.”
Kama André na Mário, wewe pia unaweza kupata msaada wa kushinda zoea la kupiga punyeto. Hata ukijikuta umetumbukia tena, usikate tamaa! Uwe na hakika kwamba unaweza kushinda vita hivyo.b
-
-
Nifanye Nini Ili Niache Kufikiria Ngono Saa Zote?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
PENDEKEZO
Ikiwa umetumbukia tena katika zoea la kupiga punyeto, endelea kupambana! Chunguza kwa makini kilichokufanya urudie zoea hilo, na ujaribu kukiepuka.
-