Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kaeni Katika Neno Langu’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • “Katikati ya Miiba” Yamaanisha Kuwa na Moyo Nusu-nusu

      15. (a) Kwa nini tuzingatie aina ya tatu ya udongo iliyotajwa na Yesu? (b) Ni nini kinachotokea hatimaye kuhusiana na udongo wa aina ya tatu, na kwa nini?

      15 Tunapaswa kuzingatia aina ya tatu ya udongo, yaani udongo wenye miiba, kwa sababu unafanana kwa njia fulani na udongo mzuri. Mbegu iliyoanguka kwenye udongo wenye miiba inatoa mizizi na kuota sawa na ile inayoanguka kwenye udongo mzuri. Mwanzoni, hakuna tofauti katika ukuzi wa mmea mpya katika aina hizi mbili za udongo. Hata hivyo, baada ya muda hali fulani inatokea ambayo hatimaye inasonga mmea. Tofauti na udongo mzuri, udongo huu umejaa miiba. Mmea mchanga unapochipuka kutoka udongoni, unasongwa na ‘miiba inayokua pamoja nao.’ Kwa muda fulani mimea hiyo inapigania lishe, nuru, na nafasi, lakini hatimaye miiba inashinda mmea huo na ‘kuusonga.’—Luka 8:7.

      16. (a) Ni watu gani wanaofanana na udongo wenye miiba? (b) Kulingana na masimulizi ya vitabu vitatu vya Injili, miiba huwakilisha nini?—Ona kielezi-chini.

      16 Ni watu gani wanaofanana na udongo wenye miiba? Yesu anaeleza hivi: “Hawa ndio ambao wamesikia, lakini, kwa kuchukuliwa na mahangaiko na mali na raha za maisha haya, wao husongwa kabisa na hawakamilishi kitu.” (Luka 8:14) Kama vile mbegu za mpanzi na miiba inavyokua katika udongo kwa wakati uleule, ndivyo watu fulani hujaribu kujifunza neno la Mungu na wakati uleule kufuatia “raha za maisha haya.” Ukweli wa neno la Mungu hupandwa katika mioyo yao, lakini unakabili ushindani kutoka kwa mambo mengine wanayohitaji kuyashughulikia. Moyo wao wa mfano umegawanyika. (Luka 9:57-62) Hilo huwazuia wasiwe na wakati wa kutosha kutafakari neno la Mungu kwa sala na kwa njia inayofaa. Wanashindwa kuvama katika neno la Mungu na hivyo wanakosa kuonyesha uthamini unaohitajiwa ili kuvumilia. Hatua kwa hatua, ufuatiaji wa mambo ya kimwili huzuia na hata ‘husonga kabisa’ mambo ya kiroho.c Wale wasiompenda Yehova kwa moyo wote wanapatwa na matokeo ya kuhuzunisha kama nini!—Mathayo 6:24; 22:37.

      17. Tunapaswa kufanya maamuzi gani maishani ili tusisongwe na miiba ya mfano inayotajwa katika kielezi cha Yesu?

      17 Kwa kutanguliza mambo ya kiroho badala ya mambo ya kimwili, tunaepuka kusongwa na matatizo na raha za ulimwengu huu. (Mathayo 6:31-33; Luka 21:34-36) Hatupaswi kupuuza kusoma na kutafakari yale tunayosoma katika Biblia. Tutapata wakati zaidi wa kutafakari kwa makini na kwa sala tukifanya maisha yetu yawe sahili kadiri tuwezavyo. (1 Timotheo 6:6-8) Watumishi wa Mungu ambao kwa njia ya mfano wameng’oa miiba kutoka kwenye udongo ili mmea unaozaa matunda upate lishe, nuru na nafasi zaidi, wanabarikiwa na Yehova. Sandra mwenye umri wa miaka 26 anasema hivi: “Ninapotafakari baraka ambazo nimepata kwa kujifunza kweli, ninaona kwamba ulimwengu hauwezi kutoa kitu chochote kinacholingana na kweli!”—Zaburi 84:11.

  • ‘Kaeni Katika Neno Langu’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • c Kulingana na masimulizi ya mfano wa Yesu katika vitabu vitatu vya Injili, mbegu inasongwa na matatizo na raha za ulimwengu huu: “Mahangaiko ya mfumo huu wa mambo,” “nguvu za udanganyifu wa mali,” “tamaa za mambo yale mengine,” na “raha za maisha haya.”—Marko 4:19; Mathayo 13:22; Luka 8:14; Yeremia 4:3, 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki