-
Inamaanisha Nini Kupenda Vitu vya Kimwili?Amkeni!—2003 | Aprili 8
-
-
Ama kweli utakubali kwamba kupenda vitu vya kimwili kunatia ndani mengi zaidi ya kuwa na mali nyingi.
-
-
Inamaanisha Nini Kupenda Vitu vya Kimwili?Amkeni!—2003 | Aprili 8
-
-
Kamusi moja inasema kwamba kupenda vitu vya kimwili ni “kukazia fikira au kujiingiza sana katika vitu vya kimwili badala ya mambo ya kiakili na ya kiroho.” Kwa hiyo, kupenda vitu vya kimwili kunatokana na mambo tunayotamani, tunayotanguliza, na kuzingatia maishani. Jambo hilo linaonyeshwa na mifano miwili ifuatayo ya Biblia.
Baruku, aliyekuwa mwandishi wa nabii Yeremia, alipewa shauri kali na Yehova. Huenda alikuwa maskini kwa sababu ya hali za Yerusalemu na kwa kushirikiana na Yeremia ambaye hakupendwa na watu wengi. Hata hivyo, Yehova alimwambia hivi: “Je, unajitafutia mambo makuu? Usiyatafute.” Huenda Baruku alianza kupenda vitu vya kimwili na kukazia fikira mali au ufanisi wa watu wengine. Yehova alimkumbusha Baruku kwamba Angemwokoa wakati wa uharibifu wa Yerusalemu uliokuwa unakaribia lakini Hangeokoa mali zake.—Yeremia 45:4, 5.
Yesu alitoa mfano wa mtu aliyekuwa anazingatia sana mambo ya kimwili. Mtu huyo alikaza fikira zake kwenye mali badala ya kuzitumia kuongeza utumishi wake kwa Mungu. Tajiri huyo alisema: “Hakika nitabomoa ghala zangu na kujenga zilizo kubwa zaidi, . . . nami hakika nitaiambia nafsi yangu: ‘Nafsi, wewe una vitu vyema vingi vilivyolimbikwa kwa miaka mingi; starehe, kula, kunywa, jifurahishe mwenyewe.’” Kisha Yesu akasema: “Lakini Mungu akamwambia, ‘Wewe mwenye kukosa akili, usiku huu wanadai nafsi yako kutoka kwako. Ni nani, basi, atakayepaswa kuwa na vitu ulivyoviweka akiba?’ Hivyo ndivyo huwa kwa mtu ajilimbikiaye hazina mwenyewe lakini si tajiri kuelekea Mungu.”—Luka 12:16-21.
Tunajifunza nini kutokana na masimulizi hayo mawili? Yanatusaidia kutambua kwamba mtu anakuwa mwenye kupenda vitu vya kimwili, si kwa sababu ya mali alizo nazo, bali kwa sababu ya kuziona kuwa muhimu sana. Mtume Paulo alisema: “Wale waazimiao kuwa matajiri huanguka ndani ya kishawishi na mtego na tamaa nyingi zisizo za akili na zenye kuumiza, ambazo hutumbukiza watu ndani ya uharibifu na uangamizo. Kwa maana kupenda fedha ni mzizi wa mambo mabaya ya namna zote, na kwa kujitahidi kufikilia kupenda huku wengine wameongozwa wapotee njia kutoka kwenye imani na wamejichoma wenyewe kotekote kwa maumivu mengi.” (1 Timotheo 6:9, 10) Matatizo hutokea mtu anapoazimia kuwa tajiri na kupenda vitu vya kimwili.
-