-
Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa MotoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Kutwaa Mlo wa Jioni”
18. Ni fursa gani ambayo Yesu anaweka mbele ya Wakristo katika Laodikia?
18 Yesu anaendelea kusema: “Tazama! Mimi ninasimama penye mlango na kubisha. Ikiwa ye-yote asikia sauti yangu na kufungua mlango, mimi nitaingia ndani ya nyumba yake na kutwaa mlo wa jioni pamoja na yeye na yeye pamoja na mimi.” (Ufunuo 3:20, NW) Ikiwa Wakristo hao Walaodikia wanamkaribisha Yesu ndani ya kundi lao, yeye atawasaidia washinde uvuguvugu wao!—Mathayo 18:20.
19. Yesu anadokeza nini anapoahidi kutwaa mlo wa jioni pamoja na kundi katika Laodikia?
19 Bila shaka mtajo wa Yesu wa mlo wa jioni unawakumbusha Walaodikia hao zile nyakati ambapo yeye alikula milo pamoja na wanafunzi wake. (Yohana 12:1-8) Sikuzote pindi hizo ziliwaletea wale waliokuwapo baraka za kiroho. Vilevile, zilikuwako pindi zisizosahaulika zilizowatia nguvu sana baada ya ufufuo wa Yesu wakati alipokuwapo kwenye mlo pamoja na wanafunzi wake. (Luka 24:28-32; Yohana 21:9-19) Kwa sababu hiyo, ahadi yake ya kuja ndani ya kundi la Laodikia na kutwaa mlo wa jioni pamoja nao ni ahadi ya kuwaletea manufaa zenye utajiri mwingi wa kiroho ikiwa tu watamkaribisha.
-
-
Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa MotoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
21. Kutoka 1919 na kuendelea, Wakristo katika kundi la kweli wameitikiaje maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Laodikia?
21 Hata ndani ya lile kundi la kweli, mmekuwamo watu mmoja mmoja ambao wako kama kinywaji ambacho si chenye moto wenye kuchochea wala chenye baridi yenye kuburudisha. Lakini Yesu angali anapenda kichangamfu kundi lake. Yeye anajifanya mwenyewe apatikane kwa Wakristo wanaoitikia kwa ukaribishaji-wageni, na wengi wamemkaribisha, kana kwamba kwa mlo wa jioni. Kama tokeo, tangu 1919 na kuendelea macho yao yamefunguliwa yaone maana ya unabii wa Biblia. Wao wamefurahia kipindi cha nuru ya elimu kubwa.—Zaburi 97:11; 2 Petro 1:19.
22. Huenda akilini Yesu alikuwa na mlo wa jioni upi wa wakati ujao, na ni nani watakaoushiriki?
22 Alipokuwa akihutubia Walaodikia, huenda Yesu akawa pia alikuwa akilini na mlo wa jioni mwingine. Baadaye katika Ufunuo tunasoma hivi: “Wenye furaha ni wale walioalikwa kwenye mlo wa jioni wa ndoa ya Mwana-Kondoo.” Hii ni ile karamu tukufu ya ushindi kwa sifa ya Yehova baada ya yeye kuwa ametekeleza hukumu juu ya dini bandia—karamu anayoishiriki Yesu pamoja na bibi-arusi wake aliyekamilika wa 144,000 katika mbingu. (Ufunuo 19:1-9, NW) Washiriki waitikivu wa hilo kundi la kale la Laodikia—ndiyo, na ndugu za Yesu Kristo waaminifu wa leo, ambao wanavaa mavazi safi ya utambulisho kuwa wao ni Wakristo wapakwa-mafuta halisi—wote watakula karamu pamoja na Bwana-arusi wao kwenye huo mlo wa jioni. (Mathayo 22:2-13) Lo! ni kichocheo chenye nguvu kama nini cha kuwa na bidii na kutubu!
-