-
Wataalamu wa Tiba wa Enzi za KatiAmkeni!—2012 | Septemba
-
-
AVICENNA, mtaalamu mwingine katika nyanja ya kitiba alitoka Bukhara, eneo ambalo sasa ni sehemu ya Uzbekistan. Alikuwa miongoni mwa wataalamu wakuu wa kitiba, falsafa, elimu ya nyota, na hisabati wa karne ya 11. Avicenna aliandika ensaiklopedia inayoitwa The Canon of Medicine, ambayo ilizungumzia mambo yote yanayohusiana na elimu ya kitiba.
Avicenna aliandika katika kitabu hicho kwamba kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza, kwamba magonjwa yanaweza kuenezwa kupitia maji na udongo, kwamba hali ya kihisia huathiri afya ya mtu, na kwamba neva hupitisha habari kuhusu maumivu na ujumbe ili misuli ijibane. Kitabu hicho kinafafanua jinsi ya kutengeneza dawa 760 tofauti—kemikali zilizomo, utendaji wake, na pia magonjwa yanayotibiwa—na akaandika kanuni zinazopaswa kufuatwa wakati wa kufanyia majaribio dawa mpya. Kitabu hicho kilitafsiriwa katika Kilatini na kikaendelea kutumiwa kwa miaka mingi sana katika shule za kitiba huko Ulaya.
-