-
Wataalamu wa Tiba wa Enzi za KatiAmkeni!—2012 | Septemba
-
-
RHAZES alizaliwa katikati ya karne ya tisa, katika jiji la kale la Rayy, ambalo sasa ni kitongoji katika jiji la Tehran. Anasemekana kuwa ndiye aliyekuwa “daktari bingwa katika eneo lote la Kiislamu na katika Enzi yote ya Kati.” Kwa ajili ya manufaa ya madaktari wengine, mwanasayansi huyo aliandika mbinu alizotumia kufanya majaribio mbalimbali, hali, vifaa alivyotumia, na matokeo aliyopata. Na aliwashauri madaktari wote kwenda sambamba na maendeleo ya kitiba katika vitengo vyao.
Rhazes alitimiza mambo mengi. Kwa mfano, maandishi yake ni sehemu ya kitabu chenye mabuku 23 kiitwacho Al-Hawi (Kitabu Chenye Habari Nyingi), ambacho ni miongoni mwa vitabu bora kabisa vya kitiba. Inasemekana kwamba kitabu hicho kinaeleza chanzo cha ukunga, elimu ya uzazi, na upasuaji wa macho. Kati ya maandishi yake 56 kuhusiana na habari za kitiba, kuna maandishi ya zamani zaidi yanayotegemeka kuhusu ugonjwa wa ndui na surua. Pia Rhazes aligundua kwamba homa ni moja ya njia ambazo mwili hujikinga.
-