Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mpinge Ibilisi na Hila Zake
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • Mwanamke akisali kwa Mungu

      Tafuta msaada wa Yehova unapokuwa mgonjwa

      17. Shetani anaweza kutumia hila gani kuwashawishi wagonjwa?

      17 Mbali na kutumia kwa ujanja tamaa yetu ya burudani, Shetani anatumia pia uhitaji wetu wa kupata matibabu. Jinsi gani? Mkristo ambaye afya yake inazidi kuzorota hata baada ya kujaribu kila njia ya kupata matibabu, anaweza kukata tamaa. (Marko 5:25, 26) Shetani na roho wake waovu wanaweza kutumia hali hiyo. Wanajua kwamba Neno la Mungu linaonya kuhusu kutafuta “usaidizi wa wale wanaozoea kufanya mambo yenye kudhuru.” (Isaya 31:2) Ili kumfanya Mkristo apuuze onyo hilo, roho waovu wanaweza kumshawishi mgonjwa ambaye hana tumaini lingine, atafute matibabu au kutumia mbinu zinazohusisha “nguvu za uchawi” au kuwasiliana na pepo—jambo ambalo ni hatari sana. Hila hiyo ya roho waovu ikifanikiwa, inaweza kudhoofisha uhusiano wake pamoja na Mungu. Kwa njia gani?

      18. Ni aina gani za matibabu ambazo Mkristo anapaswa kuepuka, na kwa nini?

      18 Yehova aliwaonya hivi Waisraeli waliogeukia “nguvu za uchawi”: “Mnaponyoosha mikono yenu, mimi huficha macho yangu kutoka kwenu. Hata mjapotoa sala nyingi, mimi sisikilizi.” (Isaya 1:13, 15) Bila shaka, sikuzote tunataka kuepuka jambo lolote linaloweza kufanya sala zetu zizuiwe na kutopata msaada kutoka kwa Yehova—hasa tunapokuwa wagonjwa. (Zaburi 41:3) Kwa hiyo, ikiwa matibabu fulani au njia ya kupima ugonjwa inahusisha mazoea fulani ya kuwasiliana na pepo, Mkristo wa kweli anapaswa kuikataa.b (Mathayo 6:13) Kwa kufanya hivyo, ataendelea kupata msaada wa Yehova.—Ona sanduku “Je, Kweli Ni Kuwasiliana na Pepo?”

      JE, KWELI NI KUWASILIANA NA PEPO?

      Kanuni: “Matendo ya mwili ni wazi, nayo ni . . . mazoea ya kuwasiliana na pepo, . . . migawanyiko, madhehebu . . . Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”—Wagalatia 5:19-21.

      Jiulize

      • Je, desturi yoyote ninayofuata inahusianishwa na imani ya dini ya uwongo?—2 Wakorintho 6:16, 17.

      • Je, kuna vitu vyovyote ninavyotumia ambavyo vinahusianishwa moja kwa moja na mazoea ya kuwasiliana na pepo?—Matendo 19:19.

      • Je, matibabu yoyote ninayopata yanatia ndani nguvu fulani zisizo za kawaida au za kichawi?—Mambo ya Walawi 19:26.

  • Mpinge Ibilisi na Hila Zake
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • b Unaweza kupata habari zaidi katika makala yenye kichwa “Mtihani wa Afya Kwako?” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 1994, ukurasa wa 19-22, na makala “Maoni ya Biblia: Uchaguzi Wako wa Matibabu—Je, Ni Muhimu?” katika toleo la Amkeni! la Januari 8, 2001.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki