-
Yote Hayo Hugharimiwaje?Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kama ilivyo kwa fasihi zao ndivyo ilivyo kwa habari ya mikutano yao. Hakuna maombi ya kuchochea hisiamoyo ili kupata fedha katika mikutano yao au kwenye mikusanyiko yao. Hakuna visahani vya michango ambavyo hupitishwa; hakuna bahasha ambazo hugawanywa za kuweka fedha; hakuna barua za kuombaomba fedha ambazo hupelekwa kwa washiriki wa makutaniko. Makutaniko hayachezi kamari au kushindania zawadi ili kupata fedha. Mapema sana kama 1894, wakati Watch Tower Society ilipotuma wasemaji wasafirio, ilitoa tangazo hili kwa manufaa ya kila mtu: “Na ieleweke tokea mwanzo kwamba kukusanya michango au njia nyinginezo za kuombaomba fedha hazikubaliwi wala kukubaliwa na Sosaiti hii.”
Hivyo, tangu mapema sana katika historia yao ya kisasa, vikaratasi vya mwaliko na mialiko mingineyo inayochapwa kwa ajili ya umma ili kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova huwa na shime “Viti Ni vya Bure. Hakuna Viingilio.”
Kuanzia mapema katika 1914, Wanafunzi wa Biblia walikodi majumba ya maonyesho pamoja na majumba mengine ya mikutano na kualika umma ili waje kuona “Photo-Drama of Creation.” Huo ulikuwa utoaji wenye sehemu nne, saa nane kwa ujumla, uliofanyizwa kwa slaidi na sinema zilizoambatanishwa na sauti. Wakati wa mwaka wa kwanza pekee, mamilioni ya watu waliuona katika Amerika Kaskazini, Ulaya, Australia, na New Zealand. Ijapokuwa baadhi ya wenyeji wa majumba ya maonyesho walitoza fedha kwa ajili ya viti vilivyohifadhiwa, Wanafunzi wa Biblia hawakuomba kamwe fedha kwa wenye kuingia ili kutazama. Na hakuna michango iliyokusanywa.
-
-
Yote Hayo Hugharimiwaje?Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kwa kufikiria hayo, maelezo yaliyotolewa na Tertuliano kuhusu mikutano iliyofanywa na watu waliojitahidi kuzoea Ukristo katika siku zake (karibu 155–baada ya 220 W.K.) lapendeza. Yeye aliandika hivi: “Hata ingawa kuna kisanduku cha aina fulani, hakikufanyizwa kwa fedha zilizolipwa zikiwa viingilio, kana kwamba dini ilikuwa jambo la mkataba. Mara moja kwa mwezi kila mtu huleta sarafu ndogo—au wakati wowote atakapo, na ikiwa tu ataka, na ikiwa aweza; maana hapana mtu alazimishwaye; ni toleo la hiari.” (Apology, 39, 5)
-
-
Yote Hayo Hugharimiwaje?Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kugharimia Mahalimahali pa Mikutano pa Kwetu
Kila kutaniko la Mashahidi wa Yehova lina visanduku vya mchango vifaavyo mahali ambapo watu waweza kuweka upaji wowote watakao—wapendapo kufanya hivyo na ikiwa wanaweza. Hushughulikiwa kwa njia ya faragha hivi kwamba kwa kawaida wengine huwa hawajui kiasi ambacho mtu anatoa. Ni jambo ambalo ni yeye na Mungu tu hujua.
-