Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa nini uhudhurie mikutano ya Kikristo?
    Amkeni!—2012 | Aprili
    • 1. UWE WA KAWAIDA

      Andiko la msingi: “Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya.”​—Waebrania 10:25, Biblia Habari Njema.

      Kwa nini ufanye kwa ukawaida jambo ambalo hufurahii kulifanya? Kwa ufupi, hiyo ndiyo siri ya kulifurahia! Fikiria jambo hili: Unawezaje kuboresha ustadi wako katika mchezo fulani​—na unawezaje kuufurahia​—ikiwa utafanya mazoezi mara chache tu? Kanuni hiyohiyo inaweza kutumiwa kuhusiana na mikutano ya Kikristo. Kadiri utakavyokuwa wa kawaida mikutanoni, ndivyo utakavyohisi kuwa hali yako ya kiroho inaimarika. Jambo hilo litafanya utamani kuendelea kuhudhuria mikutano!​—Mathayo 5:3.

      Madokezo: Baada ya kila mkutano, mwambie angalau msemaji mmoja jambo ambalo umefurahia katika hotuba aliyotoa. Andika kwenye kitabu faida moja uliyopata kwa kuhudhuria mkutano huo. Na kwa kuwa mikutano mingi huzungumzia huduma ya Kikristo, weka mradi wa kuboresha mazungumzo yako na watu wengine kuhusu imani yako. Jambo hilo litafanya habari iliyozungumziwa kwenye mikutano iwe muhimu kwako.

      “Tangu utotoni, nilizoezwa kwamba kuhudhuria mikutano ni jambo la lazima. Hata nilipokuwa mdogo, sikuwazia kwamba ningeweza kukosa mikutano. Bado nina mtazamo huo hadi leo.”​—Kelsey.

      Jambo kuu: Wale ambao ni wa kawaida mikutanoni huifurahia zaidi​—na wananufaika zaidi!

      2. SIKILIZA KWA MAKINI

      Andiko la msingi: “Kazieni uangalifu jinsi mnavyosikiliza.”​—Luka 8:18.

      Watafiti wanasema kwamba msikilizaji wa kawaida husahau asilimia 60 ya hotuba aliyosikiliza. Kama ungepoteza pesa haraka hivyo, je, hungefanya jambo fulani ili usipate hasara kubwa sana?

      Madokezo: Keti pamoja na wazazi wako karibu na jukwaa, mahali ambapo hutakengeushwa kwa urahisi. Andika mambo makuu. Ingawa kila mtu ana njia yake ya kujifunza, kuandika mambo machache kunaweza kukusaidia kumkazia msemaji fikira​—na unaweza kurudia mambo makuu baadaye.

      “Zamani, ilikuwa vigumu kwangu kusikiliza kwa makini mikutanoni, lakini sasa nimefanya maendeleo. Ninajaribu kukumbuka sababu iliyofanya nihudhurie. Si desturi tu, kama kwenda kanisani. Ninaenda mikutanoni kuabudu na kujifunza—kupata jambo fulani ninaloweza kutumia katika maisha yangu.”​—Kathleen.

      Jambo kuu: Kwenda kwenye mkutano na ukose kusikiliza kwa makini ni kama kwenda kwenye karamu halafu usile chochote.

      3. JIHUSISHE

      Andiko la msingi: “Chuma hunoa chuma, kadhalika mtu hufundishwa na wenzake.”​—Methali 27:17, BHN.

      Ukiwa kijana, unatimiza fungu muhimu katika mikutano ya kutaniko. Usidharau thamani ya kuwapo kwako na kushiriki mikutanoni, iwe ni kwa kutoa maelezo wakati wa sehemu ya maswali na majibu au iwe ni kwa kuzungumza na waamini wenzako.

      Madokezo: Jiwekee mradi wa kutoa maelezo angalau mara moja wakati wa sehemu ya maswali na majibu. Jitolee kufanya kazi ya usafi au kazi nyingine inayohitaji kufanywa kabla, wakati, au baada ya mkutano. Anzisha mazungumzo pamoja na mtu ambaye kwa kawaida hupati nafasi ya kuongea naye.

      “Nikiwa na umri wa miaka 16 hivi, nilijitolea kuzungusha mikrofoni na kutayarisha jukwaa wakati wa mikutano. Migawo hiyo ilinifanya nihisi kuwa ninahitajika, na ilinichochea kufika mapema na kutokosa mikutano. Jambo hilo lilinisaidia kupendezwa sana na mambo ya kiroho.”​—Miles.

      Jambo kuu: Usikae kitako tu​—fanya jambo fulani! Kujishughulisha mara zote kunathawabisha kuliko kuwa mtazamaji tu.

  • Kwa nini uhudhurie mikutano ya Kikristo?
    Amkeni!—2012 | Aprili
    • [Sanduku katika ukurasa wa 22]

      Chunguza ujue ni habari gani itakayozungumziwa kwenye mkutano unaofuata. Chagua sehemu moja ya mkutano inayokupendeza na . . .

      KATA NA UTOE NAKALA

      Jaza sehemu inayofuata Jaza sehemu inayofuata

      kabla ya kwenda mkutanoni. baada ya kusikiliza

      sehemu hiyo.

      Kichwa cha sehemu hiyo: Mambo niliyojifunza:

      ․․․․․ ․․․․․

      ⇩ ⇩

      Mambo ninayotaka kujua Jambo nililofurahia katika

      kuhusu habari hii: sehemu hiyo ambalo

      ninaweza kumtajia msemaji:

      ․․․․․ ․․․․․

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki