-
Mikutano ya Utumishi wa ShambaniHuduma ya Ufalme—2009 | Agosti
-
-
8. Ni katika njia zipi ambazo wale wanaohudhuria mikutano ya utumishi wa shambani wanaweza kushirikiana na wale wanaoiongoza?
8 Kuhudhuria Mkutano wa Utumishi wa Shambani: Ushirikiano ni muhimu. (Ebr. 13:17) Inapowezekana, ndugu anayeongoza kikundi atamsaidia mhubiri yeyote anayehitaji mwenzi wa kuhubiri naye. Inafaa wahubiri walio na uzoefu wahudhurie mkutano wa utumishi wa shambani ili kuwasaidia wahubiri wapya na wasio na uzoefu. Wale walio tayari kuhubiri na mtu tofauti mara kwa mara, wanaweza kutimiza mambo mengi mazuri. (Met. 27:17; Rom. 15:1, 2) Wote wanapaswa kujitahidi sana kufika kwa wakati. Ikiwa tunaheshimu mpango huu wa kiroho na tunawafikiria ndugu na dada zetu, tutachochewa kufanya marekebisho yanayohitajika kuhusiana na mkutano wa utumishi wa shambani.—2 Kor. 6:3, 4; Flp. 2:4.
-
-
Mikutano ya Utumishi wa ShambaniHuduma ya Ufalme—2009 | Agosti
-
-
10. Kwa nini inafaa wahubiri wote wa Ufalme waunge mkono kwa moyo wote mikutano ya utumishi wa shambani?
10 Kama Yesu na mitume wake walivyofanya, sehemu kubwa ya kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme inatimizwa kwa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Mikutano ya utumishi wa shambani inafanywa ili kutiana moyo na kuwa na matokeo katika huduma. Wahubiri wote wa habari njema wanapaswa kuunga mkono kadiri wawezavyo mipango yote inayohusu kazi ya kuhubiri. (Mdo. 5:42; 20:20) Sote na tuunge mkono kwa moyo wote mikutano ya utumishi wa shambani. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atatubariki sana na tunaweza kufanya moyo wa Kiongozi wetu, Yesu Kristo, ushangilie tunapohubiri habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu.—Mt. 25:34-40; 28:19, 20.
-