Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Gani Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 15
    • 7. Wakristo wa karne ya kwanza walijuaje kwamba wanastahili kushiriki mifano ya Ukumbusho?

      7 Wakristo wa kweli katika karne ya kwanza walitiwa mafuta kwa roho takatifu. Wengi wao walikuwa na zawadi moja au zaidi za kimuujiza za roho, kama vile kuongea kwa lugha mbalimbali. Kwa hiyo, haingekuwa vigumu kwao kujua kwamba walikuwa wametiwa mafuta kwa roho na hivyo walistahili kushiriki mifano ya Ukumbusho. Hata hivyo, nyakati zetu, maneno haya yaliyoandikwa kwa mwongozo wa Mungu yanaweza kumsaidia mtu kujua ikiwa yeye ni mmoja wa wale waliotiwa mafuta kwa roho: “Wote wenye kuongozwa na roho ya Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa inayosababisha hofu tena, bali mlipokea roho ya tendo la kufanywa kuwa wana, roho ambayo kwayo twapaaza kilio: ‘Abba, Baba!’”—Waroma 8:14, 15.

  • Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Gani Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 15
    • 13, 14. Kwa nini huenda watu wengine wakafikiri kimakosa kwamba wana mwito wa kimbingu?

      13 Kwa nini huenda watu wengine wakafikiri kimakosa kwamba wana mwito wa kimbingu? Wanaweza kukata tamaa ya kuishi duniani baada ya kufiwa na mwenzi wa ndoa au kupata msiba mwingine. Au huenda wakatamani kuwa na tumaini la kwenda mbinguni kama rafiki yao wa karibu anayedai kuwa Mkristo mtiwa-mafuta. Ni wazi kwamba Mungu hajampa mtu yeyote kazi ya kuwachagua wengine kwa ajili ya pendeleo hili. Naye hawatii mafuta warithi wa Ufalme kwa kufanya wasikie sauti zinazowajulisha kwamba wamechaguliwa.

      14 Huenda wengine wakadhani kwamba wana mwito wa kimbingu kwa sababu ya fundisho la dini za uwongo kwamba watu wote wazuri huenda mbinguni. Kwa hiyo, tunahitaji kujihadhari ili tusipotoshwe na maoni yenye kosa tuliyokuwa nayo zamani au na mambo mengine. Kwa mfano, huenda wengine wakajiuliza hivi: ‘Je, mimi hutumia dawa zinazoathiri hisia zangu? Je, mimi huwa na hisia nyingi mno zinazoweza kunifanya nifikirie kimakosa kuwa nimetiwa mafuta?’

      15, 16. Kwa nini watu wengine wanaweza kufikiri kimakosa kwamba wao ni watiwa-mafuta?

      15 Wengine wanaweza kujiuliza: ‘Je, ninataka kuwa mashuhuri? Je, ninajitakia makuu sasa au nina tamaa ya kuwa mrithi-mshirika wa Kristo wakati ujao?’ Warithi wa Ufalme walipoteuliwa katika karne ya kwanza, si wote walikuwa wasimamizi kutanikoni. Na wale wenye mwito wa kimbingu hawajitafutii umashuhuri wala kujigamba kwamba wametiwa mafuta. Wana sifa ya unyenyekevu tunayotarajia ionyeshwe na wale ‘walio na akili ya Kristo.’—1 Wakorintho 2:16.

      16 Huenda wengine wakafikiri kwamba wana mwito wa kimbingu kwa sababu ya kuwa na ujuzi mwingi mno wa Biblia. Lakini kutiwa mafuta kwa roho hakumfanyi mtu awe na ujuzi wa kipekee, ndiyo sababu Paulo alihitaji kuwafundisha na kuwashauri watiwa-mafuta fulani. (1 Wakorintho 3:1-3; Waebrania 5:11-14) Mungu ana mpango wa kuwapa watu wake wote chakula cha kiroho. (Mathayo 24:45-47) Kwa hiyo hakuna mtu anayepaswa kufikiri kwamba ana hekima nyingi kuliko wale wenye tumaini la kuishi duniani eti kwa sababu yeye ni Mkristo mtiwa-mafuta. Kuwa stadi katika kujibu maswali ya Kimaandiko, katika kuhubiri, au kutoa hotuba zinazotegemea Biblia hakuonyeshi kwamba mtu ametiwa mafuta kwa roho. Wakristo wenye tumaini la kuishi duniani wana ustadi huo pia.

      17. Kutiwa mafuta kwa roho hutegemea nini na nani?

      17 Mzee au Mkristo mwingine mkomavu anaweza kuzungumza na mwamini mwenzake ambaye angependa kujua mengi kuhusu mwito wa kimbingu. Hata hivyo, hakuna mtu anayeweza kumfanyia mwingine uamuzi huo. Mtu aliye na mwito huo kikweli hahitaji kuwauliza wengine ikiwa ana tumaini la kwenda mbinguni. Watiwa-mafuta ‘wamepewa uzaliwa mpya, si kupitia mbegu ya uzazi yenye kufisidika, bali kupitia isiyofisidika, kupitia neno la Mungu aliye hai na anayedumu daima.’ (1 Petro 1:23) Kupitia roho yake na Neno lake, Mungu hupanda “mbegu” inayomfanya mtu awe “kiumbe kipya,” mwenye tumaini la kwenda mbinguni. (2 Wakorintho 5:17) Yehova ndiye anayewachagua. Kutiwa mafuta ‘kwategemea, si yeye anayetaka wala yeye anayekimbia, bali Mungu.’ (Waroma 9:16) Basi mtu anawezaje kuwa na uhakika kwamba ana mwito wa kimbingu?

      Kinachowahakikishia Watiwa-Mafuta

      18. Roho ya Mungu hutoaje ushahidi pamoja na roho ya watiwa-mafuta?

      18 Ushuhuda wa roho ya Mungu huwahakikishia Wakristo watiwa-mafuta kwamba wana tumaini la kwenda mbinguni. Paulo aliandika hivi: “Mlipokea roho ya tendo la kufanywa kuwa wana, roho ambayo kwayo twapaaza kilio: ‘Abba, Baba!’ Hiyo roho yenyewe hutoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi: warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi-washirika pamoja na Kristo, mradi twateseka pamoja ili tupate pia kutukuzwa pamoja.” (Waroma 8:15-17) Chini ya mwelekezo wa roho takatifu, roho, au nia yenye nguvu ya watiwa-mafuta huwashurutisha kufuata yale ambayo Maandiko husema kuhusu wana wa kiroho wa Yehova. (1 Yohana 3:2) Roho ya Mungu huwafanya wahisi kwamba wao ni wana wa Mungu na hutia ndani yao tumaini la pekee. (Wagalatia 4:6, 7) Bila shaka wangefurahia sana kuishi milele duniani wakiwa wanadamu wakamilifu pamoja na washiriki wao wa familia na rafiki zao, lakini Mungu hajawapa tumaini hilo. Kupitia roho yake, Mungu amewapa tumaini lenye nguvu sana la kwenda mbinguni hivi kwamba wako tayari kudhabihu mahusiano yote duniani na mataraja yoyote waliyokuwa nayo.—2 Wakorintho 5:1-5, 8; 2 Petro 1:13, 14.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki