Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mlo wa Jioni wa Bwana Huadhimishwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 15
    • Ni Nani Wanaopaswa Kula na Kunywa?

      Ili kuwatambua wale wanaostahili kula na kunywa mifano ya Ukumbusho, tunahitaji kuelewa agano jipya ni nini na ni nani walio katika agano hilo. Biblia inasema: “‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda . . . Nitaitia sheria yangu ndani yao, nami nitaiandika katika moyo wao. Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. . . . Nitalisamehe kosa lao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.’”—Yeremia 31:31-34.

      Agano jipya huwawezesha wanadamu fulani wawe na uhusiano wa pekee pamoja na Yehova Mungu. Kupitia agano hilo, kikundi fulani cha watu huwa watu wake naye Yehova huwa Mungu wao. Sheria ya Yehova huandikwa ndani yao, katika mioyo yao, na hata wale ambao si Wayahudi waliotahiriwa wanaweza kuwa na uhusiano huo pamoja na Mungu kupitia agano jipya. (Waroma 2:29) Luka, mwandikaji wa Biblia, anaandika kuhusu kusudi la Mungu la ‘kuelekeza uangalifu Wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’ (Matendo 15:14) Kulingana na 1 Petro 2:10, ‘wakati mmoja wao walikuwa si watu, lakini sasa wao ni watu wa Mungu.’ Biblia huwaita “Israeli wa Mungu,” yaani, Israeli wa kiroho. (Wagalatia 6:16; 2 Wakorintho 1:21) Kwa hiyo, agano jipya ni agano kati ya Yehova Mungu na Israeli wa kiroho.

      Jioni ya mwisho akiwa pamoja na wanafunzi wake, Yesu mwenyewe pia alifanya agano lingine pamoja nao. Aliwaambia, “Nami ninafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu alivyofanya agano pamoja nami, kwa ajili ya ufalme.” (Luka 22:29) Hilo ni agano la Ufalme. Hesabu ya wanadamu wasio wakamilifu ambao wako katika agano la Ufalme ni 144,000. Baada ya kufufuliwa na kwenda mbinguni, watatawala pamoja na Kristo wakiwa wafalme na makuhani. (Ufunuo 5:9, 10; 14:1-4) Kwa hiyo, wale walio katika agano jipya pamoja na Yehova Mungu wako pia katika agano la Ufalme pamoja na Yesu Kristo. Wao tu ndio wanaostahili kula na kunywa mifano ya Mlo wa Jioni wa Bwana.

      Wale wanaostahili kula na kunywa mifano ya Ukumbusho wanajuaje kwamba wana uhusiano wa pekee pamoja na Mungu na kwamba ni warithi pamoja na Kristo? Paulo anaeleza: “Roho [takatifu] yenyewe hutoa ushahidi pamoja na roho yetu [mtazamo wetu wa akili] kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi: warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi pamoja na Kristo, mradi tu tunateseka pamoja ili pia tutukuzwe pamoja.”—Waroma 8:16, 17.

      Kupitia roho yake takatifu, au nguvu ya utendaji, Mungu huwatia mafuta wale watakaokuwa warithi pamoja na Kristo. Hilo huwahakikishia kwamba wao ni warithi wa Ufalme. Roho takatifu huwapa Wakristo waliotiwa mafuta tumaini la kuishi mbinguni. Wao huona mambo yote ambayo Biblia husema kuhusu maisha ya kimbingu kuwa yanawahusu. Isitoshe, wako tayari kudhabihu chochote kinachohusiana na maisha ya kidunia, kutia ndani uhai duniani, na pia uhusiano wote wa kibinadamu. Ingawa Wakristo watiwa-mafuta wanatambua kwamba maisha katika Paradiso ya kidunia yatakuwa mazuri, hilo si tumaini lao. (Luka 23:43) Kwa kuwa tumaini lao thabiti la kwenda mbinguni linategemea utendaji wa roho ya Mungu wala si maoni ya uwongo ya kidini, kwa kufaa Wakristo hao hula na kunywa mifano ya Ukumbusho.

      Namna gani ikiwa mtu hana uhakika kabisa kwamba yuko katika agano jipya na pia agano la Ufalme? Namna gani ikiwa roho ya Mungu haitoi ushahidi kwamba yeye ni mrithi pamoja na Kristo? Basi atakuwa amekosea kula na kunywa mifano ya Ukumbusho. Kwa kweli, Mungu hatafurahi ikiwa mtu atajifanya kimakusudi kuwa ana mwito wa kwenda mbinguni akawe mfalme na kuhani, huku akijua kabisa kwamba hakupokea mwito huo.—Waroma 9:16; Ufunuo 22:5.

  • Mlo wa Jioni wa Bwana Huadhimishwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 15
    • Je, ni lazima kula na kunywa mifano ya Ukumbusho ili kunufaika na dhabihu ya Yesu na kupokea uzima wa milele duniani? La. Biblia haidokezi popote kwamba baada ya kufufuliwa duniani, watu wenye kumwogopa Mungu kama vile Noa, Abrahamu, Sara, Isaka, Rebeka, Yosefu, Musa, na Daudi watakula na kunywa mifano hiyo. Hata hivyo, itawabidi wao pamoja na wote wanaotamani kuishi milele duniani waonyeshe imani katika Mungu na Kristo na katika uandalizi wa Yehova wa dhabihu ya fidia ya Yesu. (Yohana 3:36; 14:1) Ili kupata uzima wa milele, lazima wewe pia uonyeshe imani kama hiyo. Kuhudhuria mwadhimisho wa kifo cha Kristo kutakukumbusha dhabihu hiyo kubwa na kunapaswa kufanya uwe mwenye shukrani zaidi kwa dhabihu hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki