Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Baraka Hata Kusiwe na Uhitaji Tena”
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • WAKATI WA USAFISHAJI WA KIROHO

      3. Ni nini kilichotokea miongoni mwa watu wa kale wa Mungu kilichofanya “Israeli wa Mungu” kuchaguliwa?

      3 Karne tano baada ya siku za Malaki, Yehova, akiwakilishwa na Kristo (“mjumbe [wa Mungu] wa agano” la Abrahamu), aliingia katika hekalu halisi huko Yerusalemu ili awahukumu watu Wake wa agano. Kwa ujumla, taifa hilo halikustahili kuendelea kuwa na kibali chake, na hivyo Yehova akalikataa. (Mathayo 23:37, 38) Mambo yaliyotokea mwaka wa 70 W.K. yanathibitisha hilo. Bila shaka, Mungu alichagua “Israeli wa Mungu,” taifa la kiroho la watu 144,000 kutoka katika mataifa yote. (Wagalatia 6:16; Waroma 3:25, 26) Hata hivyo, huo haukuwa mwisho wa utimizo wa unabii wa Malaki. Unabii huo unatimizwa leo pia. Isitoshe, unabii huo unahusu tumaini lako la wakati ujao la kupata “baraka hata kusiwe na uhitaji tena.”

      4. Ni swali gani lililohitaji kujibiwa baada ya Yesu kuwekwa kuwa Mfalme katika mwaka wa 1914?

      4 Kutimizwa kwa unabii wa Biblia huthibitisha kwamba mwaka wa 1914, Yesu Kristo aliwekwa kuwa Mfalme wa Ufalme wa mbinguni wa Yehova. Kisha ukafika wakati wa Yesu kuchagua kikundi cha Wakristo waliostahili kupata kibali cha Mungu. Ni nani ambao wangethibitika kuwa safi kiroho? Jibu linapatikana katika maneno haya ya Malaki: “Ni nani atakayeistahimili siku ya kuja kwake, naye ni nani atakayesimama wakati atakapoonekana? Kwa maana atakuwa kama moto wa msafishaji.” (Malaki 3:2) Yehova alikuja wakati gani na jinsi gani katika “hekalu” lake ili kuhukumu?

      5, 6. (a) Yehova alipoingia katika hekalu lake la kiroho ili alikague, alipata hali gani miongoni mwa wengi waliodai kumwabudu? (b) Watumishi watiwa-mafuta wa Mungu walihitaji nini?

      5 Ni wazi kwamba, Mungu hakuingia katika hekalu halisi lililojengwa kwa mawe. Hekalu halisi la mwisho lililotumiwa kwa ajili ya ibada ya kweli liliharibiwa mwaka wa 70 W.K. Badala yake, Yehova aliingia katika hekalu la kiroho, mpango unaowawezesha wanadamu kumfikia na kumwabudu kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Yesu. (Waebrania 9:2-10, 23-28) Bila shaka, makanisa ya dini za Kikristo hayakuwa hekalu hilo la kiroho, kwa kuwa makanisa hayo yalikuwa sehemu ya mfumo wa kidini ulio na hatia ya kumwaga damu, kufanya ukahaba wa kiroho, na kuunga mkono mafundisho ya uwongo badala ya ibada safi. Yehova alikuwa “shahidi wa haraka juu” yao, na bila shaka walistahili hukumu kali waliyopata. (Malaki 3:5) Hata hivyo, baada ya Ufalme wa Mungu kusimamishwa, kulikuwa na kikundi cha Wakristo wa kweli katika nyua za hekalu la kiroho la Mungu. Kikundi hicho kilionyesha ushikamanifu kwa Mungu licha ya majaribu makali. Hata hivyo, watiwa-mafuta hao walihitaji pia kusafishwa. Mambo ambayo manabii wale 12 waliandika yalitaja usafishaji huo, kwa maana yalitaja ahadi zenye kutia moyo za kuwarudisha watumishi wa Mungu kiroho na kimwili. Malaki alitabiri kwamba kungekuwa na watu ambao Yehova ‘angewasafisha kama dhahabu na kama fedha.’ Watu hao ‘wangekuwa kwa Yehova watu wanaotoa toleo la zawadi katika uadilifu.’—Malaki 3:3.

      6 Kuna mambo mengi leo yanayoonyesha kwamba tangu 1918 na kuendelea, Yehova aliwasafisha Wakristo watiwa-mafuta, na kutakasa ibada, mazoea, na mafundisho yao.a Wakristo hao pamoja na “umati mkubwa” ambao ulijiunga nao baadaye, wamefaidika sana. (Ufunuo 7:9) Wakiwa kikundi chenye muungano, wanaendelea kumtolea “toleo la zawadi katika uadilifu” yaani, “lenye kumpendeza Yehova.”—Malaki 3:3, 4.

      Picha katika ukurasa wa 180, 181

      Yehova amekuwa akiwasafisha watu wake wakiwa kikundi. Je, sisi binafsi bado tunahitaji kusafishwa?

      7. Tunapaswa kujiuliza nini kuhusu msimamo wetu mbele za Mungu?

      7 Kwa ujumla, hivyo ndivyo watu wa Mungu walivyo. Hata hivyo, je, twaweza kusema vivyo hivyo kuhusu kila mmoja wetu binafsi? Huenda ukajiuliza, ‘Je, bado kuna mambo ninayohitaji kusafisha katika mtazamo na matendo yangu? Je, bado nahitaji kusafisha mwenendo wangu, kama vile Yehova alivyowasafisha watiwa-mafuta wake?’ Tuliona mwanzoni kwamba manabii hao 12 walikazia maoni na mwenendo usiofaa hali kadhalika tabia na matendo mazuri. Mambo hayo yamekusaidia kujua vizuri zaidi mambo ambayo Yehova ‘anataka kutoka kwako.’ (Mika 6:8) Ona kwamba andiko hilo linasema “kutoka kwako.” Hilo linakazia kwa nini kila mmoja wetu anapaswa kujichunguza aone ikiwa bado anahitaji kutakaswa au kusafishwa.

  • “Baraka Hata Kusiwe na Uhitaji Tena”
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • 1, 2. (a) Kila mmoja wetu anaweza kufanya maamuzi gani muhimu? (b) Tunaweza kupata baraka kutokana na utimizo wa unabii gani?

      HUU ni wakati wa hukumu na wa baraka. Ni wakati wa kuzorota kwa dini na kurudishwa kwa ibada ya kweli. Kwa kweli ungependa kupata baraka pamoja na matokeo mazuri ya sasa na ya wakati ujao yanayotokana na kurudishwa kwa ibada ya kweli! Unaweza kuwaje na hakika kuhusu mambo hayo? Jibu lapatikana katika unabii uliotimizwa kwa njia kubwa mara tu baada ya “siku za mwisho” kuanza katika mwaka wa 1914. (2 Timotheo 3:1) Malaki alitabiri hivi: “‘Bwana wa kweli [Yehova] atakuja kwenye hekalu Lake, ambaye ninyi mnamtafuta, na mjumbe wa agano mnayependezwa naye. Tazama! Atakuja hakika,’ asema Yehova wa majeshi.”—Malaki 3:1.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki