Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Habari Njema za Amani Zafika Kwenye Milima ya Chiapas
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Desemba 15
    • Matokeo ya Kuhubiri

      Mashahidi katika Jimbo la Chiapas hawakuzuiwa na magumu na hatari wasishiriki katika jitihada ya pekee ya kupelekea watu wa eneo hilo habari njema. Kwa mfano, mnamo Aprili na Mei 1995, walijiunga na Wakristo wenzao ulimwenguni pote katika kampeni ya kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 34, yenye kichwa kinachofaa Kwa Nini Maisha Yamejaa Matatizo Sana?

      Wakati wa kampeni hiyo—katika sehemu iitwayo Pueblo Nuevo, Ciro—ambaye ni painia wa kawaida, alipata familia iliyoonyesha upendezi. Aliporudi siku tatu baadaye, alianzisha funzo la Biblia pamoja na familia hiyo. Lakini Ciro aliporudi akiwa na rafiki fulani ili kuendeleza funzo na familia hiyo, mwenye nyumba hakuwako. Badala yake, kulikuwa na kikundi cha wanaume waliokuwa wamejifunika vichwa wakimngojea ili wamwumize. Walimwuliza Ciro na mwandamani wake ni nini walichokuwa wakitafuta na wakatisha kuwaua. Baada ya kusali kwa Yehova kwa ukimya, Wakristo hao wawili waliwaeleza kwa ujasiri kwamba walikuwa wamekuja kufundisha familia hiyo Biblia. Baada ya kusikia mambo hayo, wanaume hao waliojifunika vichwa waliwaachilia. Kwa sababu fulani, mwenye nyumba hakurudi nyumbani siku hiyo.

      Siku moja yapata miaka mitatu baadaye, Ciro alishangaa kumwona mwanamume huyo mlangoni pake. Ciro alifurahi kama nini kupata habari kwamba familia nzima ilikuwa imebatizwa na kwamba sasa ilikuwa ikishirikiana na kutaniko fulani nchini Guatemala! Hata mmoja wa mabinti wake alikuwa akitumikia akiwa painia wa kawaida.

  • Habari Njema za Amani Zafika Kwenye Milima ya Chiapas
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Desemba 15
    • Kijana mwingine aliyeshirikiana na harakati ya wapiganaji wa kuvizia alipewa mgawo na wakubwa wake wa kulinda doria katika eneo fulani la msituni. Alipofika kwenye jumuiya hiyo, alikuta wakazi wote, ambao wengi wao walikuwa Mashahidi wa Yehova wametoroka. Kwa hiyo akaanza kuishi katika mojawapo ya makao yaliyokuwa yameachwa. Kwa kuwa hakuwa na mengi ya kufanya, alichukua vitabu fulani alivyopata katika nyumba hiyo na kuanza kuvisoma. Vichapo hivyo vilikuwa vya Watch Tower vilivyoachwa na Mashahidi. Akiwa peke yake, kijana huyo alikuwa na wakati wa kutafakari mambo aliyokuwa akisoma. Aliamua kwamba ni lazima abadili maisha yake na kusalimisha silaha zake. Alitafuta Mashahidi haraka iwezekanavyo na kuanza kujifunza Biblia. Kwa muda wa miezi sita, alikuwa akihubiria wengine habari njema. Yeye na washiriki wengine watatu wa familia yake waliokuwa wakiunga mkono harakati ya wapiganaji wa kuvizia sasa ni Wakristo waliobatizwa.

      Kuwa na Matumaini Mema

      Hata ingawa vita hivyo vilisababisha magumu mengi, kwa kweli viliathiri ifaavyo mtazamo wa watu kuelekea kazi ya kuhubiri. Mzee mmoja katika jiji ambamo vita vilianza asimulia hivi: “Karibu siku tano baada ya vita kuanza, tulipanga kazi ya kuhubiri ndani na nje ya jiji. Watu walikuwa na hamu ya kutusikiliza. Tuliangusha vichapo vingi vya Biblia na kuanzisha mafunzo kadhaa ya Biblia. Katika eneo moja, watu wengi walikuwa wakipinga kweli, lakini kwa sababu ya vita, sasa wanasikiliza, wanajifunza Biblia, na kuhudhuria mikutano na makusanyiko.”

      Akina ndugu wanafurahi kwamba wamefaulu kuendelea na utendaji wao wa kitheokrasi licha ya hali hizo zenye wasiwasi. Wanaendelea kufanya makusanyiko yao ambayo huwajenga kiroho, licha ya kwamba jambo hilo lajulikana na wanajeshi wa serikali na wa kikundi cha EZLN. Ziara za waangalizi wasafirio pia zimekuwa kichocheo kikubwa cha kuendelea kuhubiri. Jambo linalopendeza ni kwamba, Mashahidi wanatiwa moyo hata na watu wanaohusika katika pambano hilo, ambao mara nyingi huwahimiza waendelee na kazi yao ya kuhubiri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki