Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Watu Wote Wanaalikwa!
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
    • Baada ya kuona wafanyakazi wengi wenye bidii wakimtumikia Yehova kwa furaha kwenye ofisi ya tawi huko Mexico, mwanafunzi mmoja wa Biblia ambaye ni kijana alivutiwa sana hivi kwamba akauliza: “Ninahitaji kufanya nini ili niishi hapa?” Akaambiwa: “Kwanza, ni lazima ubatizwe. Kisha, ni vizuri kutumikia ukiwa painia, yaani, mhubiri wa wakati wote wa Ufalme.” Mwanamume huyo kijana alifuata mapendekezo hayo, na miaka miwili baadaye akaalikwa kutumika katika Betheli ya Mexico, ambako amekuwa akitumikia kwa miaka 20 ambayo imepita.

  • Watu Wote Wanaalikwa!
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
    • Wengi wanaingia katika utumishi wa Betheli bila elimu yoyote ya pekee au bila ujuzi fulani wa kazi. Ndivyo ilivyokuwa kwa Abel, ambaye ametumika katika Betheli ya Mexico kwa miaka 15. Anasema hivi: “Betheli imekuwa shule halisi kwangu. Nimejifunza kuendesha mashini za kuchapisha ambazo zimetengenezwa kwa utata sana. Ninajua kwamba nikiwa na ujuzi huo, ningeweza kupata pesa nyingi sana nje ya Betheli, lakini singekuwa na maisha ninayofurahia hapa, yaani, maisha matulivu yenye kuridhisha bila mahangaiko na mashindano kama ilivyo katika kampuni nyingi za kibiashara. Ninahisi kwamba nimepata elimu bora zaidi ambayo mtu anaweza kupata, ambayo imenisaidia kukua kiroho na pia kiakili. Singeweza kupata faida hizo za kiroho hata katika chuo kikuu ambacho ni bora zaidi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki