Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ripoti ya Ulimwenguni Pote
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kazakhstan

      Katika jiji la Rudny, painia fulani alikutana na mtu anayeitwa Nikolay ambaye alisema anataka kujifunza Biblia. Lakini, kulikuwa na tatizo. Nikolay na familia yake waliishi katika kijiji cha mbali, na alikuja Rudny mara chache tu kuwatembelea watu wa jamaa yake. Ndugu huyo alimuuliza Nikolay kama angetaka amtembelee nyumbani kwake, lakini Nikolay akamweleza kwamba kijiji chao kiko umbali wa kilomita 200 kutoka Rudny na ni vigumu kukifikia.

      Hata hivyo, ndugu huyo aliandika maelekezo ya kufika kwake na kumwahidi wangekutana tena. Alipanga kutembelea kijiji hicho na akaalika ndugu mmoja na dada wawili waandamane naye. Majuma mawili baadaye walipanda gari-moshi. Walipofikia kituo cha gari-moshi kilicho karibu na kijiji cha Nikolay, waligundua kwamba walikuwa umbali wa kilomita 18 kutoka kijiji hicho, na hakukuwa na magari ya umma. Walilazimika kutembea. Hilo halikuwa jambo rahisi kwa sababu ilikuwa majira ya baridi kali na upepo ulikuwa ukivuma. Punde, tingatinga lililokuwa likisafirisha tangi la maziwa liliwapita na kusimama. Dereva aliwaambia angeweza kuwabeba ndani ya tangi! Wahubiri hao walifikiri mtu huyo anawafanyia mzaha, lakini tangi lilikuwa tupu na safi, kwa hiyo wakaingia ndani. Ijapokuwa tangi lilikuwa na baridi, angalau walikingwa na ule upepo mkali. Dereva aliwaambia angewashusha umbali wa kilomita saba kutoka kile kijiji walichokuwa wakielekea. Kutoka hapo ingewabidi kutembea kwa miguu. Iliwachukua muda wa saa mbili kutembea zile kilomita saba zilizobaki hadi kijiji cha Nikolay.

      Nikolay na mkewe Valya walishangaa na kufurahi walipowaona ndugu na dada hao mlangoni. Waliwasaidia wageni hao kupata joto na wakawapa chakula. Kisha wakazungumzia Biblia. Baada ya majuma mawili, ndugu hao kutoka Rudny walirudi kijijini humo. Yule painia anasema hivi: “Nikolay alikuja kutuchukua kwenye kituo cha gari-moshi. Wanakijiji wengi walitaka kuongea na ‘wale watu waliosafiri katika tangi la maziwa.’ Kwa hiyo, Nikolay alipanga ratiba ili wote waliopendezwa wapate nafasi ya kuzungumza nasi. Wote walioorodheshwa walifuata mpango huo na wakakubali kujifunza Biblia.” Hatimaye, karibu wote walioanza kujifunza Biblia katika kijiji hicho walifanya maendeleo ya kiroho. Miaka miwili baadaye, Nikolay na Valya walibatizwa. Sasa wana wao wawili ni wahubiri ambao hawajabatizwa, na hivi majuzi Nikolay aliwekwa kuwa mzee katika kikundi hicho cha mbali.

  • Ripoti ya Ulimwenguni Pote
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 47]

      Tulisafiri katika tangi la maziwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki