-
Wanaume—Je, Mnajitiisha Chini ya Ukichwa wa Kristo?Mnara wa Mlinzi—2010 | Mei 15
-
-
Iga Sifa za Kristo
11. (a) Tunapaswa kujitahidi sana kumwiga nani? (b) Kwa nini wanaume hasa walio katika kutaniko wanapaswa kujitahidi kumwiga Yesu?
11 Watu wote katika kutaniko la Kikristo, hasa wanaume, wanapaswa kuendelea kujitahidi kuiga sifa za Kristo. Kama tulivyoona, Biblia inatangaza hivi: “Kichwa cha kila mwanamume ni Kristo.” Wanaume Wakristo wanapaswa kujitahidi kuiga kichwa chao, Kristo, kama vile Kristo alivyomwiga Mungu wa kweli ambaye ni Kichwa chake. Mtume Paulo alifanya hivyo alipogeuka na kuwa Mkristo. Aliwahimiza Wakristo wenzake hivi: “Iweni waigaji wangu, kama vile mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.” (1 Kor. 11:1) Naye mtume Petro alisema: “Mliitwa kwenye mwendo huu, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.” (1 Pet. 2:21) Himizo la kumwiga Kristo linawahusu hasa wanaume kwa sababu nyingine. Kwa sababu hao ndio wanaowekwa kuwa wazee na watumishi wa huduma. Kama Yesu alivyopata shangwe kwa kumwiga Yehova, ndivyo wanaume Wakristo wanavyopaswa kupata shangwe katika kumwiga Kristo na sifa zake.
-
-
Wanaume—Je, Mnajitiisha Chini ya Ukichwa wa Kristo?Mnara wa Mlinzi—2010 | Mei 15
-
-
13 Wale wanaoongoza katika kutaniko ni wanaume wasio wakamilifu, na hivyo wanapaswa sikuzote kukumbuka udhaifu huo. (Rom. 3:23) Kwa hiyo, wanapaswa kuwa na hamu kubwa ya kujifunza kumhusu Yesu na kuiga upendo wake. Wanahitaji kutafakari kuhusu jinsi Mungu na Kristo wanavyoshughulika na watu na kisha wajitahidi kuwaiga. Petro anatuhimiza hivi: “Ninyi nyote jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe, kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”—1 Pet. 5:5.
14. Wazee wanapaswa kuwaheshimu wengine kwa kadiri gani?
14 Wanaume waliowekwa rasmi katika kutaniko wanapaswa kuonyesha sifa nzuri wanaposhughulika na kundi la Mungu. Andiko la Waroma 12:10 linasema hivi: “Katika upendo wa kindugu iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima iweni wa kwanza.” Wazee na watumishi wa huduma wanawaheshimu wengine. Kama Wakristo wote kwa ujumla, wanaume hao hawapaswi ‘kufanya jambo lolote kwa ugomvi au kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili wakiwaona wengine kuwa ni bora kuliko wao.’ (Flp. 2:3) Bila shaka, wale wanaoongoza wanapaswa kuwaona wengine kuwa ni bora kuliko wao. Wakifanya hivyo, wanaume hao waliowekwa rasmi watakuwa wakifuata shauri hili la Paulo: “Ingawa hivyo, sisi tulio na nguvu tunapaswa kuchukua udhaifu wa wale wasio na nguvu, na tusiwe tukijipendeza wenyewe. Kila mmoja wetu na ampendeze jirani yake katika yaliyo mema kwa ajili ya kujengwa kwake. Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe.”—Rom. 15:1-3.
-