Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
    • Mzee mmoja alisema hivi kuhusu shule hiyo: “Tunashukuru kwamba ofisi ya tawi inawatuma ndugu waliozoezwa vizuri ili watusaidie kufanya kazi ya kulichunga kundi la Mungu.” Vivyo hivyo, ofisi moja ya tawi katika Mashariki ya Mbali ilisema hivi: “Wahitimu wa shule hiyo wana huruma sana. Wanafanya kazi kwa bidii na hivyo wanaheshimiwa sana na kutaniko. Unyenyekevu, uchangamfu, na bidii yao zinajulikana na kuthaminiwa sana. Wanajitoa kwa hiari na kuhamia katika makutaniko ambayo yanahitaji wachungaji.” (Wafilipi 2:4) Wanaume kama hao wanawaburudisha waamini wenzao na wanastahili pongezi.—1 Wakorintho 16:18.

  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
    • Ofisi kadhaa za tawi zinaripoti kwamba wanaume hao, “wanafahamu vizuri mipango ya tengenezo,” “wanachukua migawo yao kwa uzito,” “wanawasaidia wengine kuelewa na kuheshimu tengenezo la Yehova,” na “wanachangia uchangamfu na hali ya kiroho ya makutaniko yao.”

  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
    • Kutumikia Katika Maeneo ya Mbali

      Wahitimu fulani waliowekwa rasmi kuwa mapainia wa pekee wanasaidia vikundi vilivyo mbali kuwa makutaniko. Akishukuru kwa msaada wao, mzee katika eneo la mbali huko Guatemala alisema hivi: “Kwa miaka 20 nilikuwa na wasiwasi kuhusu jinsi eneo hili kubwa lingehubiriwa. Mara nyingi, nilisali kuhusu jambo hilo. Ndugu kutoka katika Shule ya Mazoezi ya Kihuduma wamezoezwa vizuri kutoa hotuba na pia katika mambo ya kitengenezo, nami ninashukuru sana kuona kwamba eneo hili sasa linashughulikiwa kwa upendo.”

  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
    • Ofisi ya tawi ya Uholanzi inasema kwamba wahitimu wa Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ni “vielelezo kwa vijana wanaume ambao wanafikiria jinsi watakavyotumia maisha yao.”

  • Shule Ambayo Wahitimu Wake Wanawafaidi Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Novemba 15
    • Ofisi ya tawi ya Korea inaripoti kwamba “wahitimu zaidi ya 200 wanatimiza majukumu muhimu sana katika kusaidia makutaniko na vikundi vya lugha za kigeni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki