-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Wamishonari hao walitumwa, si ili watumikiwe, bali watumikie. Ilikuwa wazi kwa njia nyingi kwamba kwa kweli hilo ndilo walilojitahidi kufanya. Hakuna ubaya kukubali upaji wa kimwili unaotolewa kwa hiari (na si ukiwa tokeo la kuombwaombwa) kwa kuthamini msaada wa kiroho. Lakini ili kufikia mioyo ya watu katika Alaska, John Errichetti na Hermon Woodard waliona kuwa inanufaisha kuchukua angalau wakati kidogo kufanya kazi kwa mikono yao ili kuandaa mahitaji yao ya kimwili, kama vile alivyofanya mtume Paulo. (1 Kor. 9:11, 12; 2 The. 3:7, 8) Utendaji wao mkuu ulikuwa kuhubiri habari njema. Lakini walipopokea ukaribishaji-wageni, wao pia walisaidia katika kazi zilizohitaji kufanywa—kwa kielelezo, kutengeneza paa la mwanamume mmoja kwa sababu waling’amua kwamba alihitaji msaada. Na waliposafiri mahalimahali kwa mashua, walisaidia kupakua shehena. Upesi watu waling’amua kwamba wamishonari hao hawakuwa kama makasisi wa Jumuiya ya Wakristo hata kidogo.
Katika sehemu nyingine wamishonari Mashahidi walilazimika kufanya kazi ya kimwili kwa wakati fulani ili tu kujiwekea msingi katika nchi fulani ndipo waweze kuendelea na huduma yao huko. Hivyo, wakati Jesse Cantwell alipoenda Kolombia, alifundisha Kiingereza katika idara ya utabibu ya chuo kikuu hadi hali ya kisiasa ilipobadilika na vizuizi vya kidini vikaondolewa. Baada ya hapo aliweza kutumia ujuzi wake katika huduma ya wakati wote akiwa mwangalizi asafiriye wa Mashahidi wa Yehova.
-
-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika siku hizo za mapema, mara nyingi ilikuwa kawaida kwamba hakuna aliyekuwa akingoja kuwakaribisha wamishonari. Ilikuwa ni juu yao kupata mahali pa kuishi. Wakati Charles Eisenhower, pamoja na wengine 11, walipowasili Kuba katika 1943, usiku wa kwanza walilala sakafuni. Siku iliyofuata walinunua vitanda na kutengeneza makabati wakitumia kreti za matofaa. Wakitumia michango yoyote waliyopokea kwa fasihi walizoangusha, pamoja na alawansi ya kiasi iliyoandaliwa na Watch Tower Society kwa mapainia wa pekee, kila kikundi cha wamishonari kilimtegemea Yehova ili abariki jitihada zao za kulipa kodi ya nyumba, kupata chakula, na kulipa gharama nyingine muhimu.
-