-
Njia za Kupanua Huduma YakoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
mkubwa unaoongoza kwenye utendaji.” Je, sivyo ilivyo kwetu pia? Naam, tuna nafasi nyingi za kumtumikia Yehova tunaposhirikiana na kutaniko, hasa katika kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini kama Paulo, tunatambua kwamba kupita katika ‘mlango huo mkubwa’ kunahusisha kukabiliana na “wapinzani wengi.” (1 Kor. 16:9) Paulo alikuwa tayari kujitia nidhamu. Ona alivyosema: “Naupigapiga mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.” (1 Kor. 9:24-27) Je, unamwiga Paulo?
26 Kila mmoja wetu anaweza kujiwekea malengo ya kitheokrasi kulingana na hali zake. Wengi wanashiriki katika utumishi wa wakati wote kwa sababu walijiwekea malengo ya kitheokrasi mapema maishani. Walipokuwa bado watoto, wazazi wao waliwatia moyo wajiwekee malengo. Hivyo, wamefurahia baraka nyingi katika utumishi wa Yehova na hawajuti kamwe. (Met. 10:22) Malengo mengine mazuri tunayoweza kujiwekea ni kama vile kushiriki katika utumishi wa shambani kila juma, kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia, au kutenga wakati zaidi wa kutayarisha mikutano. Jambo muhimu ni kubaki washikamanifu na kutimiza huduma yetu kikamili. Tukifanya hivyo, tutamletea Yehova sifa na kufikia lengo letu kuu zaidi la kumtumikia milele.—Luka 13:24; 1 Tim. 4:7b, 8.
-
-
Mipango ya Mahali pa IbadaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 11
Mipango ya Mahali pa Ibada
WAABUDU wa kweli wa Yehova wanaamuriwa wakusanyike pamoja ili wafundishwe na watiane moyo. (Ebr. 10:23-25) Mahali pa kwanza ambapo Waisraeli, watu waliochaguliwa na Mungu, walikusanyika kwa ajili ya ibada paliitwa “hema la ibada, yaani, hema la mkutano.” (Kut. 39:32, 40) Baadaye, Sulemani mwana wa Daudi alijenga nyumba, au hekalu, kwa utukufu wa Mungu. (1 Fal. 9:3) Baada ya hekalu hilo kuharibiwa mwaka wa 607 K.W.K., Wayahudi walipanga kukutana kwenye majengo yaliyoitwa masinagogi ili kumwabudu Mungu. Baada ya muda, hekalu lilijengwa tena, na kwa mara nyingine likawa kituo cha ibada ya kweli. Yesu alifundisha kwenye masinagogi na pia hekaluni. (Luka 4:16; Yoh. 18:20) Yesu alifanya mkutano hata kwenye mlima.—Mt. 5:1–7:29.
2 Baada ya Yesu kuuawa, Wakristo walikusanyika katika sehemu za umma na kwenye nyumba za watu ili kufundisha Maandiko na kushirikiana na waamini wenzao. (Mdo. 19:8, 9; Rom. 16:3, 5; Kol. 4:15; Flm. 2) Nyakati nyingine Wakristo wa karne ya kwanza walilazimika kukutana mahali ambapo hapakuwa na watu ili kuwaepuka watesaji. Kwa kweli, zamani watumishi waaminifu wa Mungu walitamani sana kukusanyika mahali pa ibada ili ‘kufundishwa na Yehova.’—Isa. 54:13.
3 Leo pia, sehemu za umma na nyumba za watu hutumiwa kwa ajili ya mikutano ya Kikristo. Mara nyingi nyumba
-