-
“Hii Ni Siku Yenu”Mnara wa Mlinzi—2011 | Februari 1
-
-
“Mtegemee Yehova kwa Moyo Wako Wote”
Gerrit Lösch, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alizungumza na wanafunzi kuhusu kichwa hicho chenye kuchochea fikira. Alieleza jinsi ambavyo mara nyingi watu wa Mungu, wa kale na wa kisasa, wameonyesha imani yao kwa Yehova.
Katika hali inayofanana na hiyo, “wamishonari wanahitaji kuwa na imani kuhusu migawo yao,” Ndugu Lösch akaeleza. “Kwa mfano,” akasema, “mnaweza kujiuliza: ‘Je, nitaweza kujifunza lugha mpya? Je, nitaweza kuzoea utamaduni mpya? Je, nitaweza kushinda hisia ya kutamani kurudi nyumbani?’” Kuhusiana na maswali hayo Ndugu Lösch aliwahimiza wanafunzi ‘wamtegemee Yehova.’
Pia, Ndugu Lösch alisoma andiko la Methali 14:26 linalosema: “Katika kumwogopa Yehova kuna uhakika wenye nguvu.” Imani yetu katika Yehova itaimarika ikiwa tutatafakari kuhusu jinsi ambavyo ametubariki katika njia nyingi.
Biblia inasema kwamba mtu anayeweka imani yake katika Yehova “atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, unaopeleka mizizi yake kando ya mto; naye hataona joto linapoingia, bali kwa kweli majani yake yatakuwa mengi.”—Yeremia 17:7, 8.
Jambo tunalojifunza liko wazi: “Hata mkabili hali gani,” Ndugu Lösch akasema, “imani yenu inapaswa kuwa katika Yehova.”
-
-
“Hii Ni Siku Yenu”Mnara wa Mlinzi—2011 | Februari 1
-
-
“Mfanye Yehova Kuwa Mwamba wa Moyo Wako.” Akizungumzia kichwa hicho chenye kunasa fikira, kilichotegemea Zaburi 73:26, Gary Breaux, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Marekani, aliwasaidia wanafunzi kuelewa uhitaji wa kumtegemea Yehova. Yehova ni kama mwamba katika maana gani? Ndugu Breaux alisema: “Yehova anaweza kuwa chanzo cha utulivu kinachoweza kuulinda moyo wako.” Bila shaka, moyo unaweza kutupotosha tunapokabili jaribu la ustahimilivu. (Yeremia 17:9) Hali mpya ya hewa, vyakula vipya, marafiki wapya katika makao ya wamishonari—lolote kati ya mambo hayo linaweza kumfanya mtu afikirie kuacha utumishi wake. “Mtakabili hali ambazo zitawafanya mpime mambo na kufanya maamuzi,” akasema Ndugu Breaux. “Je, utafanya maamuzi yatakayomfurahisha Yehova? Ikiwa utafanya hivyo, Yehova atakuwa ‘mwamba wa moyo wako.’ Ataongoza hatua zako.”
-