Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hekima I Pamoja na Wenye Kiasi”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
    • Maoni Yenye Kiasi Kuhusu Mapendeleo Yetu

      8, 9. (a) Kwa nini tuwe na maoni yenye kiasi juu yetu wenyewe? (b) Wale ambao wana madaraka fulani wanaweza kuonyeshaje kiasi?

      8 Paulo aliwawekea Wakristo wa leo mfano mzuri. Hata tuwe tumepewa mapendeleo gani, hatupaswi kuhisi kwamba sisi ni bora kuliko wengine. “Ikiwa yeyote afikiri yeye ni kitu wakati yeye si kitu,” Paulo aliandika, “anadanganya akili yake mwenyewe.” (Wagalatia 6:3) Kwa nini? Kwa sababu “wote wamefanya dhambi na hupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Waroma 3:23; 5:12) Ndiyo, hatupaswi kusahau kwamba sisi sote tumerithi dhambi na kifo kutoka kwa Adamu. Mapendeleo ya pekee hayatuondolei hali yetu ya chini yenye dhambi. (Mhubiri 9:2) Kama Paulo, ni kwa fadhili tu isiyostahiliwa kwamba wanadamu wanaweza kuwa na uhusiano wowote pamoja na Mungu, sembuse kumtumikia katika pendeleo fulani la kipekee.—Waroma 3:12, 24.

      9 Akitambua jambo hilo, mtu mwenye kiasi hajivunii mapendeleo yake wala hajisifii mafanikio yake. (1 Wakorintho 4:7) Anapotoa mashauri au mwelekezo, anafanya hivyo kama mfanyakazi mwenzi—wala si kama bwana-mkubwa. Hakika, ingekuwa makosa kwa mtu ambaye hufanya mambo fulani kwa njia bora kutafuta sifa au kutumia vibaya heshima anayopewa na waamini wenzake. (Mithali 25:27; Mathayo 6:2-4) Sifa pekee inayofaa hutoka kwa wengine—na haipaswi kutafutwa. Na tukisifiwa, jambo hilo halipasi kutufanya tujifikirie kuliko ilivyo lazima.—Mithali 27:2; Waroma 12:3.

      10. Eleza jinsi wengine wanaoonekana kuwa wa hali ya chini wanavyoweza kuwa “matajiri wa imani” kwelikweli.

      10 Tunapokabidhiwa madaraka fulani, kuwa wenye kiasi kutatusaidia kuepuka kujifikiria mno, tukitokeza wazo la kwamba kutaniko linastawi kwa sababu ya jitihada zetu na uwezo wetu. Kwa mfano, huenda tuna kipawa cha kufundisha. (Waefeso 4:11, 12) Lakini, tukiwa wenye kiasi ni lazima tutambue kwamba baadhi ya mambo makubwa zaidi tunayojifunza kwenye mikutano ya kutaniko hayafundishwi kutoka jukwaani. Kwa mfano, je, hutiwi moyo unapoona mzazi ambaye hana mwenzi akija kwa ukawaida kwenye Jumba la Ufalme akiambatana na watoto wake? Au mtu ambaye ameshuka moyo anayehudhuria mikutano japo hisia zenye kudumu za kujiona kuwa hafai? Au kijana ambaye anazidi kufanya maendeleo ya kiroho japo mavutano mabaya shuleni na kwingineko? (Zaburi 84:10) Watu hawa huenda wasiwe mashuhuri. Mara nyingi majaribu ya uaminifu-maadili wanayokabili hayaonwi na wengine. Lakini, huenda wao ni “matajiri wa imani” kama tu wale ambao ni mashuhuri. (Yakobo 2:5) Kwani hatimaye, uaminifu ndio humfurahisha Yehova.—Mathayo 10:22; 1 Wakorintho 4:2.

  • “Hekima I Pamoja na Wenye Kiasi”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
    • Kuonyesha Kiasi na Busara

      13, 14. (a) Tunaweza kuonyeshaje kiasi tunapopata pendeleo fulani la utumishi? (b) Ndugu A. H. Macmillan aliwekaje mfano mzuri wa kuwa mwenye kiasi?

      13 Tunaweza kujifunza mengi kutokana na jinsi Gideoni alivyoonyesha kiasi. Kwa mfano, inakuwaje tunapopokea pendeleo fulani la utumishi? Je, kwanza tunafikiria umashuhuri au sifa zitakazotokezwa na pendeleo hilo? Au kwa kiasi na kwa sala tunafikiria kama tunaweza kutimiza matakwa ya mgawo huo? Ndugu A. H. Macmillan, aliyemaliza mwendo wake wa duniani mwaka wa 1966 aliweka mfano mzuri kwa habari hiyo. Pindi moja C. T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Watch Tower Society, alimwomba Ndugu Macmillan atoe maoni yake kuhusu mtu ambaye angesimamia kazi Ndugu Russell asipokuwapo. Katika mazungumzo yaliyofuata, Ndugu Macmillan hakujipendekeza hata kidogo, ijapokuwa ingekuwa rahisi sana kwake kufanya hivyo. Mwishowe, Ndugu Russell alimwomba Ndugu Macmillan afikirie kukubali mgawo huo. “Niliduwaa pale nilipokuwa nimesimama,” Ndugu Macmillan akaandika miaka mingi baadaye. “Nilifikiria jambo hilo kwa uzito sana, na kusali juu yake kwa muda fulani kabla ya kumwambia hatimaye kwamba ningefurahi kufanya yote niwezayo ili kumsaidia.”

      14 Baadaye kidogo, Ndugu Russell akafa, na ikawa kwamba Watch Tower Society haina msimamizi. Kwa kuwa Ndugu Macmillan ndiye aliyekuwa msimamizi wakati Ndugu Russell alipokuwa katika safari ya mwisho ya kuhubiri, ndugu fulani alimwambia hivi: “Mac, kuna uwezekano mkubwa kwamba ni wewe utakuwa msimamizi. Ulikuwa mwakilishi wa pekee wa Ndugu Russell wakati alipokuwa ameenda, na alituambia sisi sote tufanye yale unayotuambia. Sasa, alienda na hakurudi. Inaonekana ni wewe utaendeleza kazi hii.” Ndugu Macmillan akajibu: “Ndugu, hupaswi kufikiria mambo hayo hivyo. Hii ni kazi ya Bwana na wadhifa pekee unaopokea katika tengenezo la Bwana ni ule ambao Bwana anaona unafaa akupe; na nina hakika mimi sistahili kufanya kazi hiyo.” Kisha Ndugu Macmillan akapendekeza mtu mwingine achukue wadhifa huo. Kama Gideoni, yeye alikuwa na maoni yenye kiasi juu yake mwenyewe—na ni vizuri tusitawishe maoni kama hayo.

      15. Tunaweza kutumia ufahamu katika njia zipi zinazofaa tunapowahubiria wengine?

      15 Sisi pia tunapaswa kuwa wenye kiasi katika njia ambayo tunatekeleza mgawo wetu. Gideoni alikuwa mwenye busara, na alijaribu kutowakasirisha wapinzani wake bila sababu. Vivyo hivyo, katika kazi yetu ya kuhubiri, tunapaswa kuwa wenye kiasi na wenye busara kuhusu jinsi tunavyozungumza na wengine. Ni kweli kwamba tunapigana vita ya kiroho ya kupindua “mambo yaliyotiwa kwa nguvu sana katika mahandaki” na “mawazowazo.” (2 Wakorintho 10:4, 5) Lakini hatupaswi kuzungumza kwa kuwadharau wengine au kuwafanya wawe na sababu yoyote halali ya kuudhika na ujumbe wetu. Badala yake, ni lazima tustahi maoni yao, tukazie mambo tunayokubaliana nao, kisha tuzingatie mambo yafaayo ya ujumbe wetu.—Matendo 22:1-3; 1 Wakorintho 9:22; Ufunuo 21:4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki