Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Moldova
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • Kuanzia mwaka wa 1918 hadi 1940, Moldova ilitawaliwa na Rumania, ambayo ilikuwa ufalme wakati huo. Serikali ya Rumania ilimweka waziri wa madhehebu, ambaye aliamua mambo ya dini. Kwa sababu waziri huyo aliwaogopa viongozi wa Kanisa la Othodoksi, alipinga kazi ya Wanafunzi wa Biblia na kujaribu kuwapiga marufuku pamoja na vitabu vyao vya Biblia. Kwa hiyo, aliwashtaki ndugu kwamba walikuwa wakishirikiana na Wakomunisti.

      Kwa sababu viongozi wa serikali waliwachukia watu wa Yehova, afisa mmoja wa jeshi la Moldova alimtumia polisi fulani mkuu agizo la serikali lililoidhinishwa Aprili 25, 1925. Agizo hilo lilisema hivi: “Kupatana na Kifungu cha Polisi wa Usalama Na. 17274/925, tuna pendeleo la kukuarifu kwamba Wizara ya Mambo ya Ndani imeamua kupiga marufuku na kukomesha mahubiri ya ‘Wanafunzi wa Biblia,’ na tunataka uchukue hatua zinazohitajika ili kutimiza lengo hilo.”

      Ripoti ambayo ofisi ya Rumania ilituma kwenye makao makuu Oktoba 17, 1927, inaonyesha jinsi upinzani huo wa serikali ulivyowaathiri akina ndugu. Kwa ufupi, ripoti hiyo ilisema kwamba mikutano ya makutaniko ilikuwa imesimamishwa na kukatazwa kila mahali, na ‘mamia ya ndugu walikuwa wamefikishwa mbele ya mahakama za jeshi na za umma.’ Pia ilisema hivi: ‘Ni mikutano michache tu iliyoweza kufanywa katika majira ya kiangazi, kwa kuwa wapelelezi na polisi wa siri walipeleleza makutaniko, na bado wanayapeleleza, hasa makutaniko ya vijijini ambayo ni mengi. Mikutano mingi hufanywa misituni, mahali palipofichika vizuri.’

      Ripoti hiyo ilisema hivi pia: ‘Kazi ya waangalizi wanaosafiri ilikatizwa mwezi wa Machi. Katika mwezi uo huo, waziri wa mambo ya ndani alitoa amri kali kisiri kwamba wahudumu wa wakati wote wakamatwe na wafungwe. Punde si punde, karibu wahudumu wote wa wakati wote walikuwa wamefungwa. Ijapokuwa hatuogopi wala ndugu hawaogopi, kwa kuwa tumepata upinzani tangu kazi ilipoanzishwa katika nchi hii, wakati huu mbinu zao za kukomesha kazi ya kuhubiri ni zenye mafanikio sana hivi kwamba ni vigumu kuhubiri.’

  • Moldova
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • 1925: Kazi ya Wanafunzi wa Biblia yapigwa marufuku.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki