-
Nilimtumikia Mungu Licha ya MagumuAmkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
Kupelekwa Uhamishoni Siberia
Mnamo Aprili 1, 1951, mguu wangu ukiwa na plasta, mimi, familia yangu pamoja na Mashahidi wengine tulikamatwa na kupelekwa uhamishoni Siberia.b Hatukuwa na wakati wa kutosha kujitayarisha, hivyo tulibeba chakula kidogo tu. Baada ya muda mfupi, kikaisha.
Hatimaye, baada ya kukaa majuma mawili ndani ya gari-moshi, tulifika Asino, katika wilaya ya Tomsk. Tulishushwa kama ng’ombe. Ingawa kulikuwa na baridi kali sana, tulifurahia hewa safi. Mnamo mwezi wa Mei, theluji ilipoyeyuka, tulisafirishwa umbali wa kilometa 100 kwa meli hadi Torba, ambako kulikuwa na kambi ya kupasua mbao katika misitu ya Siberia. Tukaanza kifungo na kazi ngumu—ambacho tuliambiwa kingeendelea milele.
Ingawa kufanya kazi ngumu katika kambi ya kupasua mbao ni tofauti na kufungwa gerezani, tulikuwa tukichunguzwa daima. Wakati wa usiku tulilala pamoja katika behewa. Wakati wa kiangazi, tulijenga makao sahili ambayo kwa sehemu yalichimbiwa ardhini, ambamo tungeishi wakati wa baridi kali.
Kwa sababu ya plasta niliyokuwa nayo mguuni, nilipewa kazi ya kutengeneza misumari badala ya kufanya kazi misituni. Kazi hiyo iliniwezesha kunakili kisiri magazeti ya Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine vya Biblia. Kwa kawaida, vichapo hivyo viliingizwa kisiri katika eneo letu kutoka Ulaya magharibi, umbali wa maelfu ya kilometa.
Nakamatwa na Kufungwa
Plasta niliyokuwa nayo iliondolewa mwaka wa 1953. Licha ya kujitahidi kuwa mwangalifu, polisi wa KGB waligundua utendaji wangu wa kiroho pamoja na kazi yangu ya kunakili vichapo vya Biblia. Mwishowe, nilihukumiwa miaka 12 katika kambi ya gereza pamoja na Mashahidi wengine. Hata hivyo, wakati wa kesi, sote tulitoa ushahidi mzuri kumhusu Mungu wetu, Yehova, na makusudi yake ya upendo kwa wanadamu.
Mwishowe tulipelekwa kwenye kambi mbalimbali karibu na Irkutsk, mamia ya kilometa upande wa mashariki. Watu ambao walionwa kuwa maadui wa Serikali ya Sovieti waliteswa katika kambi hizo. Kuanzia Aprili 8, 1954, hadi mapema mwaka wa 1960, nilifungwa katika kambi 12 za kazi ngumu.
-
-
Nilimtumikia Mungu Licha ya MagumuAmkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
Mashahidi kadhaa kutoka makutaniko ya karibu walipelekwa uhamishoni huko Siberia mwaka wa 1949. Basi kwa mara nyingine tena wale waliobaki walijitahidi kuhubiri kwa uangalifu zaidi.
-
-
Nilimtumikia Mungu Licha ya MagumuAmkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
b Miisho-juma miwili ya kwanza ya Aprili 1951, Wasovieti walitekeleza mpango wa kuwakamata Mashahidi wa Yehova zaidi ya 7,000 pamoja na familia zao walioishi katika sehemu ya magharibi ya Muungano wa Sovieti na kuwasafirisha maelfu ya kilometa kwa gari-moshi upande wa mashariki hadi Siberia.
-
-
Nilimtumikia Mungu Licha ya MagumuAmkeni!—2005 | Aprili 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 21]
Gerezani, 1955
[Picha katika ukurasa wa 23]
Dada Wakristo huko Siberia, Maria (chini kushoto) alikuwa na umri wa miaka 20 hivi
-