Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nilimtumikia Mungu Licha ya Magumu
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Katika vijiji vya karibu, Mashahidi waliokataa kujiunga na jeshi la Rumania walikamatwa, na wengi wao walihukumiwa miaka 20 na kazi ngumu. Baba aliitwa kwenye kituo cha polisi na kupigwa vibaya sana kwa sababu ya kuwa Shahidi. Mimi pia nililazimishwa kutoka shuleni ili niende kanisani.

      Mambo yalibadilika wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Mnamo Machi 1944, Wasovieti waliteka mara moja sehemu ya kaskazini ya Bessarabia. Kufikia Agosti, walikuwa wameteka nchi nzima. Wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 16 hivi.

      Punde si punde, wanaume wote wakakamavu katika kijiji chetu walikuwa wameandikishwa katika jeshi la Sovieti. Lakini Mashahidi hawakujiunga na upande wowote. Kwa hiyo, walifungwa miaka kumi gerezani. Mnamo Mei 1945, Ujerumani ilisalimu amri na Vita vya Pili vya Ulimwengu vikaisha huko Ulaya. Hata hivyo, Mashahidi wengi huko Moldova walikaa gerezani hadi mwaka wa 1949.

  • Nilimtumikia Mungu Licha ya Magumu
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Mashahidi walipoendelea kuhubiri kwa bidii, wenye mamlaka walianza kuwachunguza kwa makini zaidi. Serikali ya Sovieti ilianza kupekua nyumba zetu ili kutafuta vichapo vya Biblia na kutukamata kwa sababu tulihubiri na hatukushiriki siasa wala kutumikia jeshini. Mashahidi kadhaa kutoka makutaniko ya karibu walipelekwa uhamishoni huko Siberia mwaka wa 1949. Basi kwa mara nyingine tena wale waliobaki walijitahidi kuhubiri kwa uangalifu zaidi.

  • Nilimtumikia Mungu Licha ya Magumu
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Baadaye, nilisafirishwa zaidi ya kilometa 3,000 kuelekea magharibi kwenye kambi kubwa za Mordovia za wafungwa kilometa 400 hivi kusini-mashariki mwa Moscow. Nilipata fursa ya kukutana na Mashahidi waaminifu kutoka sehemu nyingi za Muungano wa Sovieti.

      Wasovieti waligundua kwamba Mashahidi waliporuhusiwa kuchangamana na wafungwa wengine wasio Mashahidi, baadhi ya wafungwa hao pia walikuja kuwa Mashahidi. Kwa hiyo, katika magereza makubwa ya Mordovia yaliyofikia umbali wa kilometa 30 au zaidi, ambayo yalikuwa na kambi nyingi za kazi ngumu, walijaribu kututenga na wafungwa wengine. Zaidi ya Mashahidi 400 waliwekwa pamoja katika kambi yetu. Dada Wakristo wapatao 100 au zaidi walikuwa katika kambi nyingine kubwa umbali wa kilometa kadhaa.

      Nilijitahidi sana kusaidia kupanga mikutano ya Kikristo katika kambi yetu, vilevile kunakili vichapo vya Biblia ambavyo vililetwa kambini kisiri. Bila shaka wasimamizi wa kambi waligundua jambo hilo. Muda mfupi baadaye, mnamo Agosti 1961, nilihukumiwa mwaka mmoja katika gereza maarufu la Vladimir la enzi ya utawala wa Zari, kilometa 200 hivi kaskazini-mashariki mwa Moscow. Rubani Mmarekani Francis Gary Powers, ambaye alikuwa akiendesha ndege iliyopigwa risasi Mei 1, 1960, ilipokuwa ikipeleleza Urusi, alifungwa pia katika gereza hilo hadi Februari 1962.

      Nilipokuwa katika Gereza la Vladimir, nilipewa chakula kidogo tu cha kuniwezesha kuishi. Nilistahimili njaa kwa sababu nikiwa kijana nilizoea hali hiyo, lakini nilishindwa kuvumilia baridi kali sana ya mwaka wa 1961 na 1962. Mabomba ya kupasha joto gereza yaliharibika, na hivyo chumba changu kilikuwa na baridi kali kupindukia. Daktari mmoja aliona hali yangu yenye kusikitisha na kufanya mipango ili nipelekwe kwenye chumba kingine kilichokuwa afadhali katika majuma ya kwanza ya baridi kali.

      Naimarishwa Kuvumilia Magumu

      Mawazo yasiyofaa yanaweza kumvunja mtu moyo baada ya kukaa peke yake kwa miezi kadhaa, na wasimamizi wa gereza hutaka hivyo. Hata hivyo, nilisali daima nikaimarishwa na roho ya Yehova pamoja na maandiko niliyokumbuka.

      Nilipokuwa katika Gereza la Vladimir nilikumbuka maneno ya mtume Paulo kwamba “tunakazwa katika kila njia, lakini hatubanwi kupita kiasi cha kuweza kusonga,” na “tunafadhaishwa, lakini si bila njia ya kutokea kabisa.” (2 Wakorintho 4:8-10) Baada ya mwaka mmoja, nilirudishwa katika kambi kubwa ya Moldova. Nikakamilisha kifungo changu cha miaka 12 katika kambi hizo mnamo Aprili 8, 1966. Baada ya kuachiliwa huru, walisema kwamba mimi ni mtu “asiyeweza kubadilika.” Kwangu, huo ulikuwa uthibitisho wa wazi kwamba nilidumisha uaminifu wangu kwa Yehova.

      Mara nyingi nimeulizwa jinsi tulivyopata na kunakili vichapo vya Biblia katika kambi za Sovieti licha ya jitihada za kutuzuia kufanya hivyo. Si watu wengi waliojua siri hiyo, kama anavyosema mfungwa mmoja wa kisiasa kutoka Latvia ambaye alifungwa miaka minne katika kambi ya wanawake ya Potma. Aliandika hivi baada ya kufunguliwa mwaka wa 1966: “Kwa njia fulani Mashahidi waliendelea kupata vichapo vingi.” Amalizia hivi: “Ni kana kwamba malaika waliruka kambini na kudondosha vichapo hivyo.” Kwa kweli, tulitimiza kazi hiyo kwa msaada wa Mungu tu!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki