Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Meteora Miamba Mirefu Sana
    Amkeni!—2001 | Agosti 22
    • Makao ya Watawa Angani

      Haidhuru ufafanuzi wa asili ya Meteora, tangu karne ya tisa W.K., miamba hiyo imewavutia watu. Wapanda-milima wa siku hizi, wanaopanda Meteora wakiwa na vifaa maalum vya kupanda milima, waweza kutambua ustadi wa watawa wa kale waliokaa ndani ya mapango na nyufa za miamba hiyo. Mjadala juu ya jinsi makao hayo ya watawa yalivyojengwa juu ya miamba isiyoweza kufikiwa kwa urahisi ungali waendelea.

      Watu hao wa kale walitumia njia gani kupanda na kushuka kutoka kwenye makao yao yenye fahari? Naam, kama vile kitabu Meteora—The Rock Monasteries of Thessaly kinavyosema ‘huenda walipanda kwa ngazi za mbao ambazo zilishushwa kutoka juu ya majabali au wangevutwa wakiwa ndani ya neti ambayo iliteremshwa kwa kutumia chombo cha kuinua vitu kilichokuwa juu kwenye makao yao. Vyovyote vile, mgeni alihitaji tu kutumaini nia njema na ubuni huo usioaminika wa watawa wa kiume.’ Mtu mmoja aliyekuwa mkuu wa watawa alipoulizwa ni mara ngapi ile kamba iliyovuta neti ilibadilishwa, alisema hivi: ‘Inapokatika tu.’ Mwaka wa 1925 sehemu za kukanyagia zilichongwa kwenye mwamba ili iwe rahisi kupanda miamba hiyo.

      Watawa wa kwanza kupanda nguzo hizo walikuwa Varnavas, kati ya mwaka wa 950 W. K. na 965 W. K., na Andronikos kutoka Krete, mnamo mwaka wa 1020. Watawa wengine wa kiume kutoka sehemu zote za Byzantium walifuata, wakifanya idadi ya makao ya watawa yaliyo juu ya miamba yaongezeke kufikia 33. Kufikia karne ya 16 na 17, jamii hizo zilikuwa zimefikia upeo wao, lakini tangu wakati huo zimedidimia.

      “Tutazame tulivyo sasa!” akaomboleza mkuu mmoja wa makao ya watawa. “Ah, . . . vijana hawatutaki tena!” Kwa hakika, ni makao sita tu ya watawa yanayotumiwa kwa sasa. Makao mawili hukaliwa na watawa wa kike. Waweza kupata makao ya watawa yaliyoachwa ukiwa kwenye miamba kadhaa ya Meteora.

      Mandhari Yenye Utamaduni Mwingi

      Leo makao ya watawa yaliyo miambani ni mojawapo ya sehemu za kitamaduni zenye kuvutia zaidi za Ugiriki. Kwa mujibu wa Shirika la Elimu, Sayansi, na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, makao hayo ni sehemu ya kitamaduni yenye thamani sana. Hivi karibuni Serikali ya Ugiriki ilihangaikia sana kuhifadhiwa kwa utamaduni wa Meteora. Majengo yaliyorekebishwa na majumba ya makumbusho yamefunguliwa kwa ajili ya wageni. Yana nini?

      Licha ya mambo kama sanamu zinazobebeka, mavazi rasmi ya kanisa, na vitabu vya muziki, majumba hayo yana hati za Biblia zisizopatikana kwa urahisi. Kati ya hati hizo kuna hati ya ngozi ya Kodeksi 591, ya mwaka wa 861 W. K.-862 W. K., ambayo ina habari zinazofasiri kitabu cha Biblia cha Mathayo.

  • Meteora Miamba Mirefu Sana
    Amkeni!—2001 | Agosti 22
    • [Picha katika ukurasa wa 16]

      Makao ya watawa ya Mt. Nicholas Anapausas

      Makao ya watawa ya Rousanou

      [Hisani]

      M. Thonig/H. Armstrong Roberts

      [Picha katika ukurasa wa 17]

      Makao ya watawa ya Utatu Mtakatifu

      Makao ya watawa ya Great Meteoron

      [Hisani]

      R. Kord/H. Armstrong Roberts

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki