Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za Misri
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
    • Akiwa na umri wa miaka 40, wakati ambapo Musa angetazamiwa kuwa Mmisri halisi, ‘alitoka kuwaendea ndugu zake, akatazame mizigo yao.’ Mambo aliyotenda baada ya hapo yanaonyesha kwamba hakuenda kuchunguza tu hali yao; alitamani sana kuwasaidia. Alipoona Mmisri akimpiga Mwebrania, aliingilia kati, na kumwua mwonezi huyo. Tendo hilo lilionyesha kwamba moyo wa Musa ulikuwa pamoja na ndugu zake. Yaelekea mtu aliyeuawa alikuwa ofisa ambaye alikuwa akifanya kazi yake. Wamisri walitazamia Musa awe mwaminifu kwa Farao. Hata hivyo, Musa alichochewa na kupenda haki, sifa aliyoidhihirisha siku iliyofuata ambapo aligombana na Mwebrania aliyekuwa akimpiga mwenzake isivyo haki. Musa alitaka kuwakomboa Waebrania kutoka kwenye utumwa mkatili, lakini Farao alipopata habari kwamba Musa si mwaminifu kwake, alitaka kumwua. Musa alilazimika kutorokea Midiani.—Kutoka 2:11-15; Matendo 7:23-29.b

  • Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za Misri
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
    • b Akiwa mtoro huko Midiani, Musa aliwatetea wachungaji wa kike dhaifu wasinyanyaswe. Jambo hilo linaonyesha kwamba Musa alitaka sana haki ifuatwe.—Kutoka 2:16, 17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki