-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufundisha kwa Njia ya Sinema na Maonyesho ya Slaidi
Ili kusaidia wale waliokuwa wakionyesha kupendezwa na Biblia wajue ukubwa wa tengenezo la Yehova lionekanalo, sinema ilitolewa katika 1954. Sinema hiyo, The New World Society in Action, ilisaidia pia kuondoa chuki ya kijamii kuelekea Mashahidi wa Yehova.
Katika ile ambayo sasa ni Zambia, jenereta yenye kuchukulika ilihitajiwa mara nyingi ili kuonyesha sinema hiyo. Kitambaa cheupe kilichofungwa kati ya miti miwili kilitumika kuwa kiwambo. Katika Mkoa wa Barotse, chifu mkuu alitazama sinema hiyo pamoja na familia yake ya kifalme, kisha akataka ionyeshwe kwa umma. Kama tokeo, jioni iliyofuata watu 2,500 wakaiona. Jumla ya hudhurio la maonyesho ya sinema hiyo katika Zambia kwa kipindi cha miaka 17 ilizidi milioni moja. Wale waliohudhuria walisisimuliwa na yale waliyoona. Kutoka Tanganyika ya karibu (sasa ni sehemu ya Tanzania), iliripotiwa kwamba baada ya sinema hiyo kuonyeshwa, hewa ilijaa vifijo vya umati, “Ndaka, ndaka” (Asante, asante).
Baada ya sinema The New World Society in Action, sinema nyinginezo zilifuata: The Happiness of the New World Society, Proclaiming “Everlasting Good News” Around the World, God Cannot Lie, na Heritage. Kumekuwa pia maonyesho ya slaidi, pamoja na maelezo, juu ya faida yenye kutumika ya Biblia katika nyakati zetu, mashina ya kipagani ya mafundisho na mazoea ya Jumuiya ya Wakristo, na maana ya hali za ulimwengu kwa msaada wa unabii wa Biblia, pamoja na maonyesho ya slaidi kuhusu Mashahidi wa Yehova wakiwa tengenezo, yakionyesha ziara kwenye makao yao makuu ya ulimwengu, mikusanyiko yenye kusisimua katika nchi ambako walikuwa wamepigwa marufuku hapo kwanza, na pitio la historia yao ya kisasa. Maonyesho hayo yote yamesaidia watu kujua kwamba kwelikweli Yehova ana watu duniani na kwamba Biblia ni Neno Lake lililopuliziwa roho.
-
-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 481]
Maonyesho ya sinema (barani Afrika na ulimwenguni pote) yaliwawezesha watazamaji kuona kidogo ukubwa wa tengenezo la Yehova lionekanalo
-