Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Har-magedoni—Mwanzo Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • Har-magedoni—Mwanzo Wenye Furaha

      NENO “Har–Magedoni” linatokana na neno la Kiebrania Har–Magedon, au “Mlima wa Megido.” Neno hilo linapatikana kwenye andiko la Ufunuo 16:16 linalosema hivi: “Yakawakusanya pamoja mahali panapoitwa katika Kiebrania Har–Magedoni.”

  • Har-magedoni—Mwanzo Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • Je, kutajwa kwa “Mlima wa Megido” kunamaanisha kwamba Har–Magedoni itapiganwa katika mlima fulani huko Mashariki ya Kati? La. Kwanza kabisa, hakuna mlima unaoitwa hivyo—mahali Megido ya kale ilipokuwa, kuna kilima tu chenye urefu wa meta 20 hivi kando ya bonde. Isitoshe, eneo la Megido haliwezi kuwatosha “wafalme [wote] wa dunia na majeshi yao.” (Ufunuo 19:19) Hata hivyo, Megido lilikuwa eneo ambako baadhi ya vita vikali sana na vya kukata maneno katika historia ya Mashariki ya Kati vilipiganwa. Hivyo, jina Har–Magedoni linawakilisha vita vya kukata maneno, vyenye mshindi mmoja tu.—Ona sanduku “Megido Ni Mfano Unaofaa,” katika ukurasa wa 5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki