-
Mungu Ni “Mtendaji wa Mambo Makuu”—Jinsi Nilivyotambua Jambo HiloMnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 1
-
-
Kusanyiko Lililofanywa Kaskazini
Kufikia mwaka wa 1969, kazi yetu ilikuwa inapanuka kwa haraka mjini Myitkyina, kaskazini mwa Myanmar, kwa hiyo, tukaamua kufanya kusanyiko letu la kwanza katika mji huo. Hata hivyo, tatizo letu kubwa lilikuwa kuandaa usafiri kwa ajili ya Mashahidi wote waliokuwa wakiishi kusini ili waweze kufika. Tulisali kisha tukaomba kampuni ya Reli ya Myanmar ituhifadhie mabehewa sita. Tulishangaa sana ombi letu lilipokubaliwa.
Mwishowe, kila kitu kilikuwa tayari kwa ajili ya kusanyiko. Siku ambayo wajumbe walitazamiwa kufika, tulienda kwenye kituo cha gari-moshi saa sita hivi, huku tukitazamia gari-moshi liwasili mwendo wa saa 8:30 alasiri. Tulipokuwa tunangoja, msimamizi wa kituo alitupa telegramu iliyosema: “Tumeondoa mabehewa sita ya Watch Tower Society.” Alisema kuwa gari-moshi lilishindwa kuvuta mabehewa hayo lilipokuwa likipanda mlima.
Tungefanya nini? Jambo la kwanza tulilofikiria ni kupanga upya kusanyiko. Lakini hilo lingemaanisha kuomba tena vibali vya kufanya kusanyiko, na ingechukua majuma kadhaa! Tulisali kwa Yehova kwa bidii, na tulipokuwa tukifanya hivyo, gari-moshi likawasili kwenye kituo. Hatukuamini macho yetu—gari-moshi lilikuwa na yale mabehewa sita yakiwa yamejaa Mashahidi! Walikuwa wakitabasamu na kutupungia mikono. Tulipowauliza kilichokuwa kimetukia, mmoja wao alitujibu: “Waliondoa mabehewa sita lakini si yale yetu!”
-
-
Mungu Ni “Mtendaji wa Mambo Makuu”—Jinsi Nilivyotambua Jambo HiloMnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 28]
Nikisafiri kwenda kwenye kusanyiko huko Kalemyo, Burma, mwishoni mwa miaka ya 1970
-