Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Kimbilio Letu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
    • 4. Shetani, aliye “mnasa-ndege,” hutumia mbinu gani, nasi huokokaje?

      4 Mtunga-zaburi anaendelea kusema: “Maana yeye [Yehova] atakuokoa na mtego wa mwindaji [“mnasa-ndege,” “NW”], na katika tauni iharibuyo.” (Zaburi 91:3)

  • Yehova Ni Kimbilio Letu
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 15
    • 5, 6. Ni “tauni” gani ambayo imesababisha ‘uharibifu,’ na ni kwa nini watu wa Yehova hawashindwi nayo?

      5 Mtunga-zaburi anataja “tauni iharibuyo.” Kama ugonjwa wa mlipuko wenye kuambukiza, kuna jambo linalosababisha ‘uharibifu’ kwa wanadamu na kwa wateteaji wa enzi kuu ya Yehova. Kuhusiana na hilo, mwanahistoria Arnold Toynbee aliandika: “Tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu iishe, uzalendo umefanya idadi ya nchi huru iongezeke maradufu . . . Sasa wanadamu wana mwelekeo wa kuendelea kugawanyika zaidi.”

      6 Katika karne zilizopita, watawala fulani wamechochea mapigano yanayoleta migawanyiko ulimwenguni pote. Pia wametaka watu wawatukuze au watukuze mifano yao mbalimbali. Lakini Yehova hajawahi kuruhusu waaminifu wake washindwe na “tauni” kama hiyo. (Danieli 3:1, 2, 20-27; 6:7-10, 16-22) Tukiwa udugu wa ulimwenguni pote wenye upendo, tunajitoa kwa Yehova peke yake, tunadumisha msimamo wetu wa kutokuwamo kulingana na Maandiko, na tunakiri bila upendeleo kwamba “katika kila taifa mtu ambaye humhofu [Mungu] na kutenda uadilifu akubalika kwake.” (Matendo 10:34, 35; Kutoka 20:4-6; Yohana 13:34, 35; 17:16; 1 Petro 5:8, 9) Ingawa sisi Wakristo hupatwa na ‘uharibifu’ unaokuja kwa njia ya mnyanyaso, tuna shangwe na usalama wa kiroho “mahali pa siri pake Aliye juu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki