-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
na yeye ataenda nje kuongoza vibaya yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu, kukusanya hayo pamoja kwenye vita. Hesabu ya hawa ni kama mchanga wa bahari.
-
-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
21. Kwa jitihada yake ya mwisho, Shetani anaendeleaje, na kwa nini haipasi kutushangaza kwamba wengine watafuata Shetani hata baada ya Utawala wa Miaka Elfu?
21 Jitihada ya mwisho ya Shetani itakuwaje? Yeye anadanganya “yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu,” na kuyaongoza kwenye “vita.” Ni nani angeweza kuchukua upande wa Shetani baada ya miaka elfu moja ya utawala wa kitheokrasi wenye shangwe, wenye kujenga? Basi, usisahau kwamba Shetani aliweza kuongoza vibaya Adamu na Hawa wakamilifu walipokuwa wakifurahia uhai katika Paradiso ya Edeni. Na yeye aliweza kupotosha malaika wa kimbingu ambao walikuwa wameona matokeo mabaya ya uasi wa awali kabisa. (2 Petro 2:4; Yuda 6) Kwa hiyo tusishangae kwa vile baadhi ya wanadamu wakamilifu watarubuniwa wafuate Shetani hata baada ya utawala wa Ufalme wa Mungu wa miaka elfu wenye kupendeza.
22. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na usemi “yale mataifa katika kona nne za dunia”? (b) Kwa nini waasi huitwa “Gogu na Magogu”?
22 Biblia huwaita waasi hawa “mataifa katika kona nne za dunia.” Hii haimaanishi kwamba aina ya binadamu itakuwa imekwisha gawanyikana-gawanyikana tena na kuwa mataifa yaliyo pekee. Inaonyesha tu kwamba hawa watajitenga wenyewe kutoka kwa wale washikamanifu, na waadilifu wa Yehova na kudhihirisha roho ile ile mbaya ambayo mataifa yanaonyesha leo. Wao ‘watafikiria njama yenye kudhuru,’ kama alivyofanya Gogu wa Magogu katika unabii wa Ezekieli, wakiwa na mradi wa kuharibu serikali ya kitheokrasi iliyo duniani. (Ezekieli 38:3, 10-12, NW) Kwa sababu hiyo, wao huitwa “Gogu na Magogu.”
-