Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye Tamati
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Mkusanyo Kuelekea Har–Magedoni

      25. (a) Yohana anatuambia nini juu ya semi chafu zilizovuviwa, zilizo kama vyura? (b) Kumekuwaje na msiba wenye kunyarafisha kama wa vyura wa ‘semi chafu zilizovuviwa’ katika siku ya Bwana, na tokeo likiwa nini?

      25 Yohana anatuambia: “Na mimi nikaona semi chafu tatu zilizovuviwa ambazo zilionekana kama vyura zinatoka katika kinywa cha drakoni na katika kinywa cha hayawani-mwitu na katika kinywa cha nabii bandia. Kwa hakika, hizo ni semi zilizovuviwa na roho waovu na hufanya ishara, nazo hutoka kwenda kwa wafalme wa dunia nzima yote inayokaliwa, kukusanya wao pamoja kwenye vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 16:13, 14, NW) Katika siku ya Musa Yehova alileta tauni makuruhu ya vyura juu ya Misri ya Farao, hivi kwamba “bara likaanza kuvunda.” (Kutoka 8:5-15, NW) Wakati wa siku ya Bwana, kumekuwako pia msiba wenye kunyarafisha kama wa vyura, ingawa ni kutoka chimbuko tofauti. Ndani ya huo mna ‘semi chafu zilizovuviwa’ za Shetani, kwa wazi zikifananisha propaganda zinazokusudiwa kuongoza kwa werevu watawala wote wa kibinadamu, “wafalme,” katika kumpinga Yehova Mungu. Hivyo Shetani anahakikisha kwamba wao hawaathiriwi na kule kumiminwa kwa mabakuli ya kasirani ya Mungu bali kwa imara wao wako upande wa Shetani wakati “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote” inapoanza.

      26. (a) Propaganda ya kishetani hutoka kwenye machimbuko gani matatu? (b) “Nabii bandia” ni nini, nasi tunajuaje?

      26 Hiyo propaganda huja kutoka kwa “drakoni” (Shetani) na “hayawani-mwitu” (mpango wa Shetani wa kisiasa wa kidunia), viumbe ambavyo tumekwisha kupata habari zavyo katika Ufunuo. Ingawa hivyo, huyu “nabii bandia” ni nini? Huyu ni mja-leo kwa jina tu. Wakati uliopita, sisi tulionyeshwa hayawani-mwitu wa pembe mbili mithili ya mwana-kondoo ambaye alifanya ishara mbele ya hayawani-mwitu mwenye vichwa saba. Kiumbe huyu mwenye kudanganya alitenda kama nabii kwa ajili ya huyo hayawani-mwitu. Aliendeleza ibada ya hayawani-mwitu, hata akasababisha mfano wake ujengwe. (Ufunuo 13:11-14, NW) Huyu hayawani-mwitu mwenye pembe mbili mithili ya mwana-kondoo lazima awe ndiye yule yule “nabii bandia,” anayetajwa hapa. Kuthibitisha hili, sisi tunasoma baadaye kwamba “nabii bandia” kama hayawani-mwitu wa ufananisho mwenye pembe mbili, “alifanya mbele [ya hayawani-mwitu mwenye vichwa saba] ishara ambazo kwa hizo yeye aliongoza vibaya wale ambao walipokea alama ya hayawani-mwitu na wale ambao hutoa ibada kwa mfano wake.”—Ufunuo 19:20, NW.

  • Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye Tamati
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na hizo [semi zilizovuviwa na roho waovu] zikakusanya wao [wafalme wa kidunia, au watawala] pamoja kwenye mahali ambapo huitwa kwa Kiebrania Har–Magedoni.” (Ufunuo 16:16, NW) Jina hili, ambalo wengi zaidi hufasiri Armagedoni hutokea mara moja tu katika Biblia. Lakini limechochea wazo la aina ya binadamu. Viongozi wa ulimwengu wameonya juu ya uwezekano wa Armagedoni ya nyukilia. Armagedoni imefungamanishwa pia na jiji la kale la Megido, mahali pa vita vingi vya kukata maneno katika nyakati za Biblia, na kwa hiyo baadhi ya viongozi wa kidini wamekisiakisia kwamba ile vita ya mwisho duniani itapiganwa mahali hapo padogo. Katika hili, wako mbali sana na ukweli.

      32, 33. (a) Badala ya kuwa mahali halisi, jina Har–Magedoni, au Armagedoni, huwakilisha nini? (b) Ni semi gani nyingine za Biblia zinazofanana na “Har–Magedoni” au zinazohusiana nayo? (c) Utakuwa wakati gani kwa malaika wa saba kumimina bakuli la mwisho kabisa la kasirani ya Mungu?

      32 Neno hili Har–Magedoni lamaanisha “Mlima wa Megido.” Lakini badala ya kuwa mahali halisi, linawakilisha hali ya ulimwengu ambayo ndani yayo mataifa yote yanakusanywa katika upinzani na Yehova Mungu na ambapo mwishowe yeye atawaharibu. Hii ni ya kadiri ya kuenea tufe lote. (Yeremia 25:31-33; Danieli 2:44) Inafanana na “shinikizo kubwa la divai ya kasirani ya Mungu” na “uwanda-bonde wa uamuzi,” au “uwanda-bonde wa Yehoshafati,” ambamo mataifa yanakusanywa yakauawe na Yehova. (Ufunuo 14:19; Yoeli 3:12, 14, NW) Inahusiana pia na “udongo wa Israeli” ambako majeshi ya kishetani ya Gogu wa Magogu yanaharibiwa na kata iliyo “kati ya bahari tukufu na mlima mtakatifu wa Urembo” ambako mfalme wa kaskazini anakuja “njia yote mpaka mwisho wake” mikononi mwa Mikaeli mwana-mfalme mkuu.—Ezekieli 38:16-18, 22, 23; Danieli 11:45–12:1, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki