Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tutatembea Katika Jina la Yehova Milele!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 15
    • Yehova Anyoosha Mambo

      15. Unaweza kuelezaje kwa maneno yako mwenyewe unabii wa Mika 4:1-4?

      15 Tunapofikiria unabii huo, tunaona kwamba sasa Mika anatoa ujumbe wa tumaini wenye kusisimua. Tunapata maneno yenye kutia moyo kama nini katika Mika 4:1-4! Mika anasema: “Itakuwa katika siku za mwisho ya kwamba mlima wa nyumba ya BWANA utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi. . . . Naye atafanya hukumu kati ya watu wa kabila nyingi, naye atawakemea [‘atayanyoosha mambo kuhusu,’ NW] mataifa wenye nguvu walio mbali; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.

  • Tutatembea Katika Jina la Yehova Milele!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 15
    • 16, 17. Andiko la Mika 4:1-4 linatimizwaje leo?

      16 Ni nani hao “watu wa mataifa” na “mataifa wenye nguvu” wanaotajwa hapo? Hao si mataifa na serikali za ulimwengu huu. Badala yake, unabii huo unahusu watu mmoja-mmoja kutoka katika mataifa yote ambao wamejiunga na utumishi mtakatifu kwenye mlima wa Yehova wa ibada ya kweli.

      17 Kupatana na unabii wa Mika, hivi karibuni watu wote duniani watafuata kikamili ibada safi ya Yehova. Leo, watu ‘walio na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele’ wanafundishwa njia za Yehova. (Matendo 13:48) Yehova anafanya hukumu na kunyoosha mambo kiroho kwa waamini wanaounga mkono Ufalme. Wataokoka “dhiki kubwa” wakiwa sehemu ya “umati mkubwa.” (Ufunuo 7:9, 14) Kwa kuwa wamefua panga zao kuwa majembe, hata leo watu hao wanaishi kwa amani pamoja na Mashahidi wenzao na watu wengine. Inafurahisha kama nini kuwa kati yao!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki