-
Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa NuruMnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
-
-
Kwa sababu ya bidii hiyo mpya ya Wakristo hao, wengine walivutwa kwenye nuru ya Yehova. Mwanzoni, wapya waliokuja walitiwa mafuta ili wawe washiriki wa Israeli wa Mungu. Katika Isaya 60:3 wanaitwa wafalme, kwa kuwa wataurithi Ufalme wa kimbingu wa Mungu pamoja na Kristo. (Ufunuo 20:6) Baadaye, umati mkubwa wa kondoo wengine walivutwa kwenye nuru ya Yehova. Hao ndio “mataifa” yanayotajwa katika unabii huo.
-
-
Yehova Awaremba Watu Wake kwa Kuwapa NuruMnara wa Mlinzi—2002 | Julai 1
-
-
10 Je, unaweza kuwazia furaha ya Sayuni watoto wake wanapomjia? Na bado Yehova anampa Sayuni sababu nyingine za kushangilia. Tunasoma hivi: “Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, na moyo wako utatetemeka na kukunjuka; kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, utajiri wa mataifa utakuwasilia.” (Isaya 60:5) Kwa kupatana na maneno hayo ya unabii, tangu miaka ya 1930, Wakristo wengi wenye tumaini la kuishi duniani, wamemwendea Sayuni. Wametoka katika “bahari” ya wanadamu wasio na kibali cha Mungu, nao ndio utajiri wa mataifa. Wao ni “vitu vinavyotamaniwa na mataifa [“vya mataifa,” NW].” (Hagai 2:7; Isaya 57:20) Ona pia, kwamba “vitu [hivyo] vinavyotamaniwa” hawaendi zao wakamtumikie Yehova kila mtu kivyake. Bali wao huongeza uzuri wa Sayuni wanapokuja kuabudu pamoja na ndugu zao waliotiwa mafuta, na hivyo kuwa “kundi moja” lenye “mchungaji mmoja.”—Yohana 10:16.
-