-
Urithi Wetu Wenye Thamani—Wamaanisha Nini Kwako?Mnara wa Mlinzi—2000 | Septemba 1
-
-
Kwa kuwa Abrahamu hakumzuilia mwanaye mwenyewe, Yehova alitangaza hivi: “Katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.” (Mwanzo 22:15-18) Hilo lilionyesha kwamba Mbegu iliyotajwa kwenye Mwanzo 3:15, mkombozi aliye Mesiya, angekuja kupitia uzao wa Abrahamu. Ni urithi wenye thamani kama nini kupitisha!
-
-
Urithi Wetu Wenye Thamani—Wamaanisha Nini Kwako?Mnara wa Mlinzi—2000 | Septemba 1
-
-
14, 15. (a) Baada ya kifo cha Yesu, mataifa yalianzaje kujibarikia kupitia “mbegu” ya Abrahamu? (b) Washiriki wa “Israeli wa Mungu” wanapokea urithi gani?
14 Taifa lililopewa Ufalme ni “Israeli wa Mungu,” Israeli wa kiroho, wafuasi wa Yesu Kristo 144,000 waliozaliwa kwa roho. (Wagalatia 6:16; Ufunuo 5:9, 10; 14:1-3) Baadhi ya 144,000 hao walikuwa Wayahudi halisi, lakini wengi wao walikuwa watu wa mataifa. Kwa hiyo ahadi ambayo Yehova Mungu alimtolea Abrahamu kwamba kupitia “mbegu” yake mataifa yote yangebarikiwa, ikaanza kutimia. (Matendo 3:25, 26; Wagalatia 3:8, 9) Katika utimizo huo wa kwanza, watu wa mataifa walitiwa mafuta na roho takatifu, naye Yehova akawafanya kuwa wana wa kiroho, ndugu za Yesu Kristo. Kwa hiyo, wao pia wakawa sehemu ya pili ya ile “mbegu.”—Wagalatia 3:28, 29.
-
-
Urithi Wetu Wenye Thamani—Wamaanisha Nini Kwako?Mnara wa Mlinzi—2000 | Septemba 1
-
-
18. Ahadi ya Yehova ya kwamba mataifa yote yatajibarikia yenyewe kupitia “mbegu” ya Abrahamu inatimizwaje leo?
18 Yaelekea kwamba idadi kamili ya Israeli wa kiroho, lile “kundi dogo” la warithi wa Ufalme, imetimia. (Luka 12:32) Kwa makumi ya miaka sasa, Yehova amekazia fikira kukusanywa kwa umati mkubwa wa wengine wanaotoka katika mataifa yote. Kwa hiyo, ahadi ya Yehova kwa Abrahamu ya kwamba kupitia “mbegu” yake mataifa yote yangejibarikia, yatimizwa katika njia kubwa. Waliobarikiwa wanashangilia kutoa utumishi mtakatifu kwa Yehova na kutambua kwamba wokovu wao wategemea imani katika Mwana-kondoo wa Mungu, Yesu Kristo. (Ufunuo 7:9, 10) Je, wewe umeukubali mwaliko wenye neema wa Yehova ili uwe sehemu ya kikundi hicho chenye furaha?
-