Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Siku ya Jumapili asubuhi, Oktoba 7, 1934, saa tatu, kila kikundi cha Mashahidi katika Ujerumani kilikusanyika. Walisali ili kupata mwongozo na baraka za Yehova. Kisha kila kikundi kikapeleka barua kwa maofisa wa serikali ya Ujerumani wakijulisha azimio lao imara la kuendelea kumtumikia Yehova. Kabla ya kutawanyika, walizungumzia pamoja maneno ya Bwana wao, Yesu Kristo, kwenye Mathayo 10:16-24. Baada ya hayo walienda kutoa ushahidi kwa majirani wao kuhusu Yehova na Ufalme wake chini ya Kristo.

  • “Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 694]

      Taarifa Madhubuti kwa Serikali ya Nazi

      Mnamo Oktoba 7, 1934, barua ifuatayo ilipelekwa kwa serikali ya Ujerumani na kila kutaniko la Mashahidi wa Yehova katika Ujerumani:

      “KWA MAOFISA WA SERIKALI:

      “Neno la Yehova Mungu, kama lilivyoandikwa katika Biblia Takatifu, ndiyo sheria kuu zaidi, na kwetu sisi hilo ndilo mwongozo wetu pekee kwa sababu ya kujitoa kwetu kwa Mungu na sisi ni wafuasi wa kweli na wenye moyo mweupe wa Kristo Yesu.

      “Wakati wa mwaka uliopita, na kinyume cha sheria ya Mungu na kwa kuvunja haki zetu, mmetukataza sisi tukiwa Mashahidi wa Yehova kukutana pamoja ili kujifunza Neno la Mungu na kumwabudu na kumtumikia. Katika Neno lake yeye hutuamuru sisi kwamba tusiache kukusanyika pamoja. (Waebrania 10:25) Kwetu sisi Yehova aamuru: ‘Nyinyi ni mashahidi wangu kwamba mimi ni Mungu. Nendeni mkawaambie watu ujumbe wangu.’ (Isaya 43:10, 12; Isaya 6:9; Mathayo 24:14) Kuna hitilafiano la moja kwa moja kati ya sheria yenu na sheria ya Mungu, na kwa kufuata mwongozo wa mitume waaminifu, ‘twapaswa kumtii Mungu badala ya watu,’ na hilo tutafanya. (Matendo 5:29) Kwa hiyo hii ni kuwajulisha kwamba hata iweje tutatii amri za Mungu, tutakutana pamoja kwa ajili ya funzo la Neno lake, na tutaabudu na kumtumikia kama alivyoamuru. Ikiwa serikali yenu au maofisa wenu watufanyia jeuri kwa sababu tunamtii Mungu, basi damu yetu itakuwa juu yenu na mtatoa jibu kwa Mungu Mweza Yote.

      “Hatuhusiki na mambo ya kisiasa, bali tumejitoa kikamili kwa ufalme wa Mungu chini ya Kristo Mfalme wake. Hatutamjeruhi au kumuumiza yeyote. Tungefurahi kukaa kwa amani na kufanya mema kwa watu wote kwa kadiri tupatavyo nafasi, lakini, kwa kuwa serikali yenu na maofisa wayo yaendelea katika jitihada zenu za kutulazimisha tusitii sheria ya juu zaidi ya ulimwenguni pote, tunashurutika kuwajulisha sasa kwamba, kwa fadhili yake, tutamtii Yehova Mungu na kumtumaini Yeye kabisa aweze kutuokoa kutoka uonevu wote na wenye kuonea.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki