Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kudumisha Imani Chini ya Mnyanyaso wa Kimabavu
    Amkeni!—2000 | Septemba 22
    • “Huko Ujerumani sisi huwapiga risasi Mashahidi wa Yehova. Je, waiona ile bunduki?” ofisa wa Gestapo akasema huku akiashiria bunduki iliyokuwa pembeni. “Naweza kukudunga kwa singe yake bila kuhisi majuto yoyote.”

      Nilikuwa na umri wa miaka 15 tu nilipokabili tisho hilo wakati wa kumilikiwa kwa nchi yangu na Wanazi katika mwaka wa 1942.

  • Kudumisha Imani Chini ya Mnyanyaso wa Kimabavu
    Amkeni!—2000 | Septemba 22
    • Kuhojiwa na Gestapo

      Wajerumani walianza kumiliki mwaka wa 1941, na licha ya tisho la kuadhibiwa, tuliendelea na utendaji wetu wa Kikristo. Nilianza kupainia mwaka uliofuata kwa kutumia baiskeli. Muda si muda nilikutana na Gestapo Wajerumani kama inavyoelezwa kwenye utangulizi. Mambo yalitendeka hivi.

      Siku moja nilipokuwa nikirejea nyumbani kutoka katika huduma, niliwatembelea Wakristo wenzangu wawili, mama na binti yake. Mume wa binti huyo alipinga imani yetu na alikuwa na hamu ya kutaka kujua mke wake alipokea vichapo vya Biblia kutoka wapi. Siku hiyo nilikuwa nimebeba si vichapo tu bali pia ripoti ya utumishi ya Wakristo wenzangu. Huyo mume aliniona nilipokuwa nikiondoka kutoka nyumba ile.

      “Simama!” akasema kwa hasira. Niliunyakua mfuko wangu na kukimbia.

      “Simama! Mwizi!” akapaaza sauti. Watu waliokuwa wakifanya kazi kwenye mashamba walifikiri lazima iwe nilikuwa nimeiba kitu fulani, hivyo wakanishurutisha kusimama. Mwanamume huyo alinipeleka hadi kituo cha polisi ambapo tulimkuta ofisa wa Gestapo.

      Yule ofisa kuona tu vile vichapo vilivyokuwa ndani ya mfuko wangu, alifoka kwa Kijerumani na kusema: “Rutherford! Rutherford!” Sikuhitaji mfasiri anieleze sababu ya hasira yake. Jina la Joseph F. Rutherford, aliyekuwa hapo awali msimamizi wa Watch Tower Bible and Tract Society, lilikuwa kwenye ukurasa wa pili wa vichapo vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kisha yule mwanamume alitoa shtaka la kuwa mimi nilikuwa mpenzi wa mke wake. Polisi na yule ofisa wa Gestapo waliona shtaka hilo kuwa la upuuzi kwa sababu mke wake alikuwa na umri wa kutosha kuwa mama yangu. Kisha wakaanza kunihoji.

      Walitaka kujua mimi nilikuwa nani, ninaishi wapi, na hasa nilitoa wapi vichapo hivyo. Lakini nilikataa kuwaambia. Walinipiga mara kadhaa na kunidhihaki, halafu wakanifungia ndani ya chumba kilicho chini ya ardhi. Nilihojiwa kwa siku tatu zilizofuata. Halafu nikapelekwa katika ofisi ya yule ofisa wa Gestapo aliyetisha kunidunga kwa singe. Sikujua kama angefanya alivyotishia. Niliinamisha kichwa changu na kukawa kimya. Kisha akasema ghafula: “Waweza kwenda.”

      Kama unavyoweza kung’amua, ilikuwa vigumu sana kuhubiri na pia kufanya mikutano yetu siku hizo. Tuliadhimisha Ukumbusho wa kila mwaka wa kifo cha Kristo katika Aprili 19, 1943, katika vyumba viwili vya nyumba moja huko Horyhliady. (Luka 22:19) Kabla tu ya kuanza mkutano wetu, tulisikia onyo kwamba polisi walikuwa wakija kwenye nyumba hiyo. Baadhi yetu tulijificha kwenye bustani, lakini dada yangu Anna na wanawake wengine watatu waliteremka kwenye chumba kilichokuwa chini ya ardhi. Polisi waliwapata huko na kuburuta mmoja baada ya mwingine kutoka huko ili kuwahoji. Waliteswa kwa masaa mengi, na mmoja wao alijeruhiwa vibaya.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki