Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wanazi Hawakufaulu Kunibadili
    Amkeni!—2011 | Agosti
    • Kwa sababu mimi na ndugu zangu tulikataa kabisa kutoa salamu ya heil Hitler, Baba aliagizwa afike kortini. Aliambiwa atie sahihi hati fulani kuonyesha kwamba ameikana imani yake. Hati hiyo pia ilimwagiza awalee watoto wake kulingana na sera za Nazi. Kwa sababu alikataa kutia sahihi hati hiyo, yeye na Mama walinyang’anywa watoto wao, nami nikatumwa katika kituo kimoja cha kuelimisha watu upya kilichokuwa kilomita 40 hivi kutoka nyumbani.

      Nilitamani sana kurudi nyumbani na nililia sana. Nikiwa huko, yule aliyekuwa akitutunza alijaribu kunilazimisha nijiunge na Kikundi cha Vijana cha Hitler, lakini nikakataa. Wasichana wengine walijaribu kuinua mkono wangu wa kulia ili niisalimu bendera ya Nazi, lakini hawakufaulu. Nilihisi kama watumishi wa Mungu wa kale waliosema: “Ni jambo lisilowaziwa, kwa upande wetu, kumwacha Yehova ili kuitumikia miungu mingine.”—Yoshua 24:16.

      Wazazi wangu walizuiwa wasinitembelee. Hata hivyo, tulikutana kisiri nilipokuwa nikienda shuleni na pia nilipokuwa shuleni. Pindi hizo zilinitia moyo sana niendelee kuwa mwaminifu kwa Yehova. Pindi moja tulipokutana, Baba alinipa Biblia ndogo, nami nikaificha vizuri kitandani mwangu. Nilifurahia sana kuisoma, ingawa nilifanya hivyo kisiri. Siku moja, karibu nipatikane nikisoma Biblia hiyo, lakini niliificha haraka chini ya blanketi.

      Napelekwa Kwenye Makao ya Watawa

      Kwa kuwa jitihada zote za kunielimisha upya hazikufua dafu, wenye mamlaka walishuku kwamba bado nilikuwa nikiwasiliana na wazazi wangu. Hivyo, mnamo Septemba (Mwezi wa 9) 1942, nilisafirishwa kwa gari-moshi hadi Munich, Ujerumani, na nikatiwa katika shule ya Wakatoliki iliyoitwa Adelgunden, ambayo pia ilikuwa makao ya watawa wa kike. Nilipokuwa nikipelekwa huko, watawa waliiona Biblia yangu na wakaichukua

  • Wanazi Hawakufaulu Kunibadili
    Amkeni!—2011 | Agosti
    • Kwa sababu mimi na ndugu zangu tulikataa kabisa kutoa salamu ya heil Hitler, Baba aliagizwa afike kortini. Aliambiwa atie sahihi hati fulani kuonyesha kwamba ameikana imani yake. Hati hiyo pia ilimwagiza awalee watoto wake kulingana na sera za Nazi. Kwa sababu alikataa kutia sahihi hati hiyo, yeye na Mama walinyang’anywa watoto wao, nami nikatumwa katika kituo kimoja cha kuelimisha watu upya kilichokuwa kilomita 40 hivi kutoka nyumbani.

      Nilitamani sana kurudi nyumbani na nililia sana. Nikiwa huko, yule aliyekuwa akitutunza alijaribu kunilazimisha nijiunge na Kikundi cha Vijana cha Hitler, lakini nikakataa. Wasichana wengine walijaribu kuinua mkono wangu wa kulia ili niisalimu bendera ya Nazi, lakini hawakufaulu. Nilihisi kama watumishi wa Mungu wa kale waliosema: “Ni jambo lisilowaziwa, kwa upande wetu, kumwacha Yehova ili kuitumikia miungu mingine.”—Yoshua 24:16.

      Wazazi wangu walizuiwa wasinitembelee. Hata hivyo, tulikutana kisiri nilipokuwa nikienda shuleni na pia nilipokuwa shuleni. Pindi hizo zilinitia moyo sana niendelee kuwa mwaminifu kwa Yehova. Pindi moja tulipokutana, Baba alinipa Biblia ndogo, nami nikaificha vizuri kitandani mwangu. Nilifurahia sana kuisoma, ingawa nilifanya hivyo kisiri. Siku moja, karibu nipatikane nikisoma Biblia hiyo, lakini niliificha haraka chini ya blanketi.

      Napelekwa Kwenye Makao ya Watawa

      Kwa kuwa jitihada zote za kunielimisha upya hazikufua dafu, wenye mamlaka walishuku kwamba bado nilikuwa nikiwasiliana na wazazi wangu. Hivyo, mnamo Septemba (Mwezi wa 9) 1942, nilisafirishwa kwa gari-moshi hadi Munich, Ujerumani, na nikatiwa katika shule ya Wakatoliki iliyoitwa Adelgunden, ambayo pia ilikuwa makao ya watawa wa kike. Nilipokuwa nikipelekwa huko, watawa waliiona Biblia yangu na wakaichukua.

      Hata hivyo, nilikuwa nimeazimia kuendelea kushikilia imani yangu kwa hivyo nilikataa kuhudhuria ibada kanisani. Nilipomwambia mmoja wa watawa kwamba wazazi wangu walikuwa na zoea la kunisomea Biblia kila Jumapili, alifanya jambo lililonishangaza. Alinirudishia Biblia yangu! Inaonekana kwamba yale niliyomwambia yalimgusa moyo. Hata aliniruhusu nimsomee Biblia hiyo.

      Pindi moja, mwalimu fulani aliniambia hivi: “Hermine, una nywele zenye rangi ya dhahabu, na macho ya bluu. Kwa hiyo, wewe ni Mjerumani, si Myahudi. Yehova ni Mungu wa Wayahudi.”

      Nilimjibu: “Lakini Yehova ndiye aliyefanya kila kitu. Yeye ndiye Muumba wa kila mtu!”

      Mwalimu mkuu pia alijaribu kunishinikiza. Wakati mmoja, aliniambia: “Hermine, mmoja wa ndugu zako amejiunga na jeshi. Unapaswa kufuata mfano wake mzuri!” Nilijua kwamba mmoja wa ndugu zangu alikuwa amejiunga na jeshi, lakini sikuwa na nia yoyote ya kufuata mfano wake.

      “Mimi si mfuasi wa ndugu yangu,” nilimwambia. “Mimi ni mfuasi wa Yesu Kristo.” Mwalimu huyo mkuu alitisha kunipeleka kwenye hospitali ya watu walio na matatizo ya akili, hata akamwagiza muuguzi ajitayarishe kunipeleka. Hata hivyo, hakufanya hivyo.

      Katika majira ya kiangazi ya mwaka wa 1943, Munich ilishambuliwa kwa mabomu, na watoto kutoka shule ya Adelgunden wakahamishwa hadi sehemu za mashambani. Wakati wa kipindi hicho, mara nyingi nilitafakari maneno ya Mama: “Iwapo siku moja tutatenganishwa na hutapokea barua zozote kutoka kwangu, kumbuka kwamba Yehova na Yesu wako pamoja nawe. Hawatakuacha kamwe. Kwa hiyo, endelea kusali.”

      Naruhusiwa Kurudi Nyumbani

      Mnamo Machi (Mwezi wa 3) 1944, nilirudishwa Adelgunden, ambako mara nyingi, iwe mchana au usiku tulijificha mahali fulani kwa sababu mji wa Munich ulikuwa ukishambuliwa sana kwa mabomu yaliyorushwa kutoka angani. Wazazi wangu waliomba mara nyingi kwamba nirudishwe nyumbani. Mwishowe ombi lao lilikubaliwa, na niliwasili nyumbani mwishoni mwa Aprili (Mwezi wa 4) 1944.

      Nilipoenda kumuaga mwalimu mkuu, aliniambia hivi: “Hermine, tuandikie barua utakapofika nyumbani. Na udumishe msimamo wako.” Mtazamo wa mwalimu huyo ulikuwa umebadilika kama nini!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki