-
Kelele—Yale Uwezayo Kufanya KuihusuAmkeni!—1997 | Novemba 8
-
-
Kelele ikiwa imeenea sana hivyo, watu wengi kwa kawaida hawatambui wanapowasumbua wengine. Ikiwa wangejua, wengine bila shaka wangeacha kufanya huo utendaji wenye kuudhi. Ni kwa sababu hii kwamba kumwendea jirani mwenye kelele kwa njia yenye urafiki kwaweza kusaidia. Mtu mmoja alikasirika kwa sababu ya malalamiko rasmi ya majirani wake kuwa alikuwa mwenye kelele. Alisema: “Nilifikiri kuwa wangekuja kwangu moja kwa moja kuniona ikiwa walikasirishwa na kelele hiyo.” Mama aliyeandaa karamu kwa ajili ya watoto fulani wachanga alishangaa alipokabiliwa na ofisa mmoja akichunguza lalamiko kuhusu kelele hiyo. “Ingekuwa bora kama waliolalamika wangeubisha mlango wangu na kuniambia ikiwa hawakufurahi,” yeye akaonelea. Basi, haishangazi kuwa ofisa mmoja Mwingereza wa afya ya kimazingira alishangaa kugundua kwamba asilimia 80 ya wale wanaolalamika kuhusu kelele ya nyumbani hawajawahi kuwaomba majirani wao wapunguze kelele.
Kujizuia kwa watu kuzungumza na majirani wao wenye kelele huonyesha ukosefu wa staha kati yao. ‘Nikitaka kucheza muziki wangu, naweza. Ni haki yangu!’ ndilo jibu watarajialo kupata na mara nyingi ndilo wapatalo. Wanaogopa kuwa pendekezo la fadhili la kupunguza sauti laweza kuongoza kwenye makabiliano ikiwa jirani mwenye kelele aona lalamiko lao kuwa lisilofaa. Ni wonyesho mbaya kama nini wa jumuiya ya wakati wa sasa! Ni kama tu taarifa ya Biblia kwamba katika hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” watu kwa ujumla watakuwa ‘wenye kujipenda wenyewe, wenye kiburi, wakali, na wenye vichwa vigumu’!—2 Timotheo 3:1-4.
Yategemea sana jinsi mhasiriwa anavyomwendea. Gazeti Woman’s Weekly lilitoa hali ifuatayo ya jinsi ya kutatua hali yenye uvutano baada ya lalamiko lenye uchokozi kukosa kufaulu: “Kwa njia yenye uchangamfu na yenye kueleweka waweza kusema, ‘Nasikitika—nilikasirika sana lakini mimi huwa mchovu sana ninapokosa kulala’ labda ndilo tu lihitajiwalo ili kupatana tena na [majirani wenye kujitetea].” Huenda ikawa watasogeza vyombo vyao vya sauti kutoka kwenye ukuta unaowaunganisha na labda kupunguza sauti kwa njia fulani.
Kwa uhalisi, ni kwenye manufaa kudumisha mahusiano mazuri na majirani wako. Mamlaka za serikali za mahali fulani hutoa huduma za upatanisho ili kuwapatanisha majirani wanaopingana. Kwa kufikiria hisia zenye uhasama ambazo malalamishi rasmi husababisha, kuita ofisa wa kutekeleza sheria kwapaswa kuonwa kuwa “jambo la mwisho kabisa mengine yote yakishindwa.”
Ikiwa watazamia kuhamia makao mapya, utaona likiwa jambo la hekima kuchunguza vyanzo viwezekanavyo vya usumbufu wa kelele kabla ya kutamatisha kandarasi. Mawakala wa uuzaji wa nyumba wapendekeza kwamba utembelee mahali unapotarajia kuishi katika saa tofauti za siku ili uchunguze kelele. Waweza kuwauliza majirani maoni yao. Ukikabiliwa na matatizo baada ya kuhamia makao yako mapya, jaribu kuyatatua kwa njia yenye ujirani. Kwenda mahakamani kwa kawaida huchochea uhasama.
-
-
Kelele—Yale Uwezayo Kufanya KuihusuAmkeni!—1997 | Novemba 8
-
-
Jinsi Uwezavyo Kuepuka Kuwa Jirani Mwenye Kelele
● Wafikirie majirani wako unapofanya jambo lenye kelele, na uwajulishe mapema.
● Shirikiana unapoombwa na jirani upunguze kelele.
● Tambua ya kwamba furaha yako haipaswi kumletea jirani yako msononeko.
● Kumbuka kwamba kelele na mitikiso hupitishwa kwa urahisi kupitia kumbi na sakafu.
● Weka vitu vya nyumbani vyenye kelele juu ya vitu vyororo.
● Hakikisha kuwa mtu aweza kuitwa kushughulikia ving’ora vya nyumba na gari viliavyo kiaksidenti.
● Usifanye kazi zenye kelele au kutumia mashine zenye kelele usiku sana.
● Usicheze muziki kwa sauti itakayowaudhi majirani wako.
● Usiwaache mbwa wakiwa peke yao kwa vipindi virefu.
● Usiwaruhusu watoto kurukaruka kwenye sakafu na hivyo kuwasumbua watu wanaoishi chini.
● Usipige honi, kugongesha milango, au kungurumisha injini ya gari usiku.
-