-
Waaminifu na Wenye Ujasiri-Japo Mnyanyaso wa NaziMnara wa Mlinzi—2000 | Aprili 1
-
-
Marufuku—Lakini Wenye Kutenda Hata Zaidi
Mnamo Mei 10, 1940, jeshi la Nazi lilishambulia Uholanzi kwa ghafula. Kwa kuwa vichapo vilivyogawanywa na Mashahidi wa Yehova vilifichua matendo maovu ya Unazi na kutetea Ufalme wa Mungu, wafuasi wa Nazi walijaribu kukomesha mara moja utendaji wa Mashahidi. Katika muda unaopungua majuma matatu baada ya Nazi kushambulia Uholanzi, walitoa amri ya siri ya kuwapiga marufuku Mashahidi wa Yehova. Mnamo Machi 10, 1941, gazeti moja lilitangaza hadharani marufuku hiyo, likiwashutumu Mashahidi kwa kupinga “taifa na makanisa.” Hivyo, msako wa Mashahidi ukaongezeka.
Jambo la kutokeza ni kwamba, ingawa kikosi chenye sifa mbaya cha Gestapo, au polisi wa siri, kilipeleleza makanisa yote, kilinyanyasa kikatili shirika moja tu la Kikristo. “Mnyanyaso hadi kifo,” asema mwanahistoria Mholanzi Dakt. Louis de Jong, “ulikipata kikundi kimoja tu cha kidini—Mashahidi wa Yehova.”—Het Koninkrik der Nederlanden in de Tweede Wereldoorlog (Ufalme wa Uholanzi Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili).
Polisi wa Gestapo walishirikiana na polisi wa Uholanzi katika kuwasaka na kuwakamata Mashahidi. Isitoshe, mwangalizi mmoja asafiriye ambaye alishikwa na hofu na kuasi imani aliwapasha wafuasi wa Nazi habari kuhusu wale waliokuwa waamini wenzake. Kufikia mwisho wa Aprili 1941, Mashahidi 113 walikuwa wamekamatwa. Je, shambulio hilo kali lilikomesha kazi ya kuhubiri?
Jibu lapatikana katika ile iitwayo Meldungen aus den Niederlanden (Ripoti Kutoka Uholanzi), hati ya siri ambayo Sicherheitspolizei (Polisi wa Usalama) wa Ujerumani waliandika mnamo Aprili 1941. Ripoti hiyo yasema hivi kuhusu Mashahidi wa Yehova: “Madhehebu hiyo iliyopigwa marufuku inaendelea na utendaji wenye bidii katika nchi yote, ikifanya mikutano na kubandika karatasi zinazotangaza maneno kama ‘Kunyanyasa Mashahidi wa Mungu ni uhalifu’ na ‘Yehova atawaadhibu wanyanyasaji kwa uharibifu wa milele.’” Majuma mawili baadaye polisi haohao waliripoti kwamba “licha ya Polisi wa Usalama kuchukua hatua kali zaidi dhidi ya utendaji wa Wanafunzi wa Biblia, utendaji wao unaendelea kuongezeka.” Naam, licha ya hatari ya kukamatwa, Mashahidi waliendelea na kazi yao, wakiwagawia watu vichapo zaidi ya 350,000 katika mwaka wa 1941 pekee!
-
-
Waaminifu na Wenye Ujasiri-Japo Mnyanyaso wa NaziMnara wa Mlinzi—2000 | Aprili 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 26]
Makala iliyotolewa katika gazeti la habari ikionyesha amri ya kupiga marufuku Mashahidi wa Yehova
-