Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Suala jingine lililohusu Mashahidi wa Yehova katika Ulaya, pamoja na sehemu nyingine za dunia, ni kutokuwamo kwa Kikristo. Kwa sababu dhamiri zao za Kikristo hazingewaruhusu kujihusisha katika mapambano kati ya wenye kuzozana wa ulimwengu, walihukumiwa kufungwa gerezani katika nchi moja baada ya nyingine. (Isa. 2:2-4) Jambo hilo liliwatoa vijana kwenye huduma yao ya kawaida ya nyumba hadi nyumba. Lakini tokeo moja lenye manufaa lilikuwa ule ushahidi mwingi uliotolewa kwa wanasheria, mahakimu, maofisa wa kijeshi, na walinzi wa gereza. Hata wakiwa gerezani Mashahidi walipata njia fulani za kuhubiri. Ijapokuwa walitendwa kinyama katika baadhi ya magereza, Mashahidi waliofungwa katika gereza la Santa Catalina katika Cádiz, Hispania, waliweza kutumia baadhi ya saa zao kutoa ushahidi kwa barua. Na katika Sweden utangazaji mwingi ulifanywa kuhusu njia ambayo kesi zilizohusu kutokuwamo kwa Mashahidi wa Yehova zilishughulikiwa. Hivyo, kwa njia nyingi watu walijulishwa juu ya uhakika wa kwamba Yehova ana mashahidi duniani na kwamba wao hushikamana kwa imara na kanuni za Biblia.

  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 495]

      Mashahidi waliokuwa gerezani katika Cádiz, Hispania, waliendelea kuhubiri kwa kuandika barua

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki