-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1940/1941, majeshi ya Ugiriki yalivamia upande wa kusini wa Albania na kuwalazimisha watu wajiunge nao. Katika kijiji kimoja ndugu fulani alipokataa, akisema kwamba haungi mkono upande wowote, askari-jeshi walishika nywele zake na kuanza kumburuta na kumpiga mpaka akazirai.
“Ungali mkaidi?” ofisa-msimamizi akamuuliza kwa hasira ndugu huyo alipopata fahamu.
“Bado siungi mkono upande wowote!” akajibu ndugu huyo.
Askari hao wakiwa wametamauka, wakamwacha aende zake.
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
WATAWALA WAPYA—MAJARIBU YALEYALE
Katikati ya mapigano na machafuko ya vita, pole kwa pole Chama cha Kikomunisti cha Albania kilikuwa kikipata umaarufu, licha ya jitihada za serikali ya Kifashisti. Mwaka wa 1943, askari-jeshi waliokuwa wakipigana na Wakomunisti walimkamata ndugu mmoja, wakamtupa ndani ya lori, wakampeleka vitani, na kumkabidhi bunduki. Akaikataa.
Kamanda akamfokea, “Wewe ni Mkomunisti! Kama ungekuwa Mkristo, ungepigana sawa tu na makasisi!”
Kamanda huyo akawaamuru askari-jeshi wamuue ndugu huyo. Walipokuwa tayari kufyatua risasi, ofisa mwingine akafika na kuuliza ni nini kinachoendelea. Alipoambiwa msimamo wa ndugu huyo, alitangua amri hiyo, naye ndugu huyo akaachiliwa.
-