-
Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
“Mpatanishi wa Agano Jipya”
11, 12. Daraka la Yesu akiwa Mpatanishi ni la pekee jinsi gani?
11 Soma 1 Timotheo 2:5, 6. Yesu ndiye yule “mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu.” Yeye ni “mpatanishi wa agano jipya.” (Ebr. 9:15; 12:24) Hata hivyo, Musa anaitwa pia mpatanishi, yaani, mpatanishi wa agano la Sheria. (Gal. 3:19) Hivyo basi, daraka la Yesu akiwa Mpatanishi ni la pekee jinsi gani?
12 Neno la lugha ya awali linalotafsiriwa “mpatanishi” ni neno la kisheria. Linamhusu Yesu akiwa Mpatanishi wa kisheria (au, katika maana fulani, wakili) wa agano jipya ambalo liliwezesha kuzaliwa kwa taifa jipya, “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:16) Taifa hilo linafanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta, ambao wanakuwa “ukuhani wa kifalme” wa kimbingu. (1 Pet. 2:9; Kut. 19:6) Agano la Sheria ambalo Musa alikuwa mpatanishi wake, halikuweza kutokeza taifa kama hilo.
13. Daraka la Yesu akiwa Mpatanishi linatia ndani nini?
13 Daraka la Yesu akiwa Mpatanishi linatia ndani nini? Yehova anatumia thamani ya damu ya Yesu kwa wale wanaoingizwa katika agano jipya. Katika njia hiyo, Yehova anawapa kisheria haki ya kuwa waadilifu. (Rom. 3:24; Ebr. 9:15) Kisha, Mungu anawaona kuwa wanastahili kuingia katika agano jipya wakiwa na tumaini la kuwa wafalme na makuhani wa kimbingu! Akiwa Mpatanishi wao, Yesu anawasaidia wadumishe msimamo safi mbele za Mungu.—Ebr. 2:16.
14. Kwa nini Wakristo wote, hata wakiwa na tumaini gani, wanapaswa kuthamini kabisa daraka la Yesu akiwa Mpatanishi?
14 Namna gani wale ambao hawamo katika agano jipya, wale ambao wanatumaini kuishi milele duniani, si mbinguni? Ingawa si washiriki wa hilo agano jipya, wao wanafaidika nalo. Wanasamehewa dhambi zao na wanatangazwa kuwa waadilifu na kuwa marafiki wa Mungu. (Yak. 2:23; 1 Yoh. 2:1, 2) Iwe tuna tumaini la kuishi mbinguni au duniani, kila mmoja wetu ana sababu nzuri ya kuthamini daraka la Yesu akiwa Mpatanishi wa agano jipya.
-
-
Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
◼ Mpatanishi wa Agano Jipya. (1 Tim. 2:5, 6) Akiwa Mpatanishi wa kisheria, Yesu aliwezesha kuanzishwa kwa taifa jipya, “Israeli wa Mungu,” linalofanyizwa na Wakristo ambao watakuwa “ukuhani wa kifalme” wa kimbingu.—Gal. 6:16; 1 Pet. 2:9.
-