-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
VITA YA MWISHO
20. Malaika afafanuaje vita ya mwisho ya mfalme wa kaskazini?
20 Ushindani kati ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini—uwe wa kijeshi, kiuchumi, au mwingineo wowote—wakaribia kwisha. Akifunua kinaganaga juu ya pambano lililo mbele, malaika wa Yehova asema hivi: “Habari zitokazo mashariki [“macheo ya jua,” NW] na kaskazini zitamfadhaisha [mfalme wa kaskazini]; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi.
-
-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
22. Ni maswali gani yanayozuka juu ya shambulio la mwisho la mfalme wa kaskazini?
22 Hata hivyo, twajua hatua ambayo mfalme wa kaskazini atachukua hivi karibuni. Akichochewa na ‘habari zitokazo macheo ya jua na kaskazini,’ atapanga vita ili “kuwaondolea mbali watu wengi.” Vita hiyo itapiganwa dhidi ya nani? Nazo ni “habari” gani zinazochochea shambulio hilo?
ASHTUSHWA NA HABARI ZENYE KUSUMBUA
23. (a) Ni tukio gani lenye kutokeza ambalo lazima litukie kabla ya Har–Magedoni? (b) “Wafalme watokao macheo ya jua” ni akina nani?
23 Fikiria jambo ambalo kitabu cha Ufunuo chasema juu ya mwisho wa Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli. Kabla ya “vita ya siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote,” Har–Magedoni, adui huyo mkubwa wa ibada ya kweli “atachomwa kabisa kwa moto.” (Ufunuo 16:14, 16; 18:2-8) Kuharibiwa kwake kuliwakilishwa na kumwagwa kwa bakuli la sita la hasira ya kisasi ya Mungu kwenye mto wa ufananisho wa Eufrati. Mto huo wakauka ili “njia ipate kutayarishwa kwa ajili ya wafalme watokao macheo ya jua.” (Ufunuo 16:12) Wafalme hao ni nani? Si wengine ila Yehova Mungu na Yesu Kristo!—Linganisha Isaya 41:2; 46:10, 11.
24. Ni tendo gani la Yehova ambalo huenda likamsumbua mfalme wa kaskazini?
24 Kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa kwafafanuliwa kinaganaga kwenye kitabu cha Ufunuo, kinachotaarifu hivi: “Pembe kumi ulizoziona [wafalme wanaotawala katika wakati wa mwisho], na hayawani-mwitu [Umoja wa Mataifa], hawa watamchukia kahaba na watamfanya ukiwa na kuwa uchi, na watakula kabisa sehemu zake zenye nyama na watamchoma kabisa kwa moto.” (Ufunuo 17:16) Kwa nini wafalme watamharibu Babiloni Mkubwa? Kwa sababu ‘Mungu atia ndani ya mioyo yao ili watekeleze fikira yake.’ (Ufunuo 17:17) Mfalme wa kaskazini ni mmoja wa watawala hao. Huenda habari asikiazo kutoka “macheo ya jua” zarejezea tendo hilo la Yehova, atiapo ndani ya mioyo ya viongozi wa kibinadamu fikira ya kumwangamiza kahaba huyo mkubwa wa kidini.
25. (a) Lengo la pekee la mfalme wa kaskazini ni nini? (b) Mfalme wa kaskazini “ataweka hema zake za kifalme” wapi?
25 Lakini mfalme wa kaskazini ataelekeza hasira yake yenye kisasi mahali fulani pa pekee. “Ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari [“bahari kuu,” NW] na mlima mtakatifu wa uzuri,” asema malaika. Wakati wa Danieli bahari kuu ilikuwa Meditarenia nao mlima mtakatifu ulikuwa Zayoni, ambapo hekalu la Mungu lilikuwa wakati mmoja. Kwa hiyo, katika utimizo wa unabii huo, mfalme wa kaskazini aliyekasirishwa apanga vita dhidi ya watu wa Mungu. Katika maana ya kiroho, mahali palipo ‘kati ya bahari kuu na mlima mtakatifu’ pawakilisha makazi ya kiroho ya watumishi wa Yehova watiwa-mafuta. Wametoka kwenye “bahari” ya wanadamu waliotengwa na Mungu nao wana tumaini la kutawala kwenye Mlima Zayoni wa kimbingu pamoja na Yesu Kristo.—Isaya 57:20; Waebrania 12:22; Ufunuo 14:1.
26. Kama inavyoonyeshwa na unabii wa Ezekieli, huenda habari ‘itokayo kaskazini’ yatokana na nani?
26 Ezekieli, aliyeishi wakati mmoja na Danieli, alitabiri pia juu ya shambulio dhidi ya watu wa Mungu “katika siku za mwisho.” Alisema kwamba uhasama huo ungeanzishwa na Gogu wa Magogu, yaani, Shetani Ibilisi. (Ezekieli 38:14, 16) Kwa njia ya kitamathali, Gogu atokea upande gani? “Pande za mwisho za kaskazini,” asema Yehova, kupitia Ezekieli. (Ezekieli 38:15) Hata shambulio hilo liwe kali namna gani, halitawaharibu watu wa Yehova. Tukio hilo lenye kutokeza litamfanya Yehova achukue hatua ili kuyaangamiza majeshi ya Gogu. Kwa hiyo, Yehova amwambia Shetani hivi: ‘Nitakutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa.’ “Nitakupandisha toka pande za mwisho za kaskazini; nami nitakuleta juu ya milima ya Israeli.” (Ezekieli 38:4; 39:2) Kwa hiyo, habari ‘itokayo kaskazini’ ambayo yamkasirisha mfalme wa kaskazini lazima iwe yatokana na Yehova. Lakini Mungu tu ndiye atakayeamua habari kamili zitokazo ‘macheo ya jua na kaskazini’ zitakuwa nini, nao wakati utafunua.
-