Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hakuna Mkaaji Atakayesema, Mimi Mgonjwa”
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Uponyaji

      20. Watu wa Mungu watapata uponyaji gani, nao wataupata lini?

      20 Sehemu hii ya unabii wa Isaya yamalizia kwa ahadi yenye kusisimua: “Hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.” (Isaya 33:24) Ugonjwa anaoutaja Isaya ni wa kiroho hasa, kwa maana wahusianishwa na dhambi, au “uovu.” Katika utimizo wa kwanza wa maneno hayo, Yehova aahidi kwamba baada ya kuachiliwa kwao kutoka utekwani Babiloni, taifa hilo litaponywa kiroho. (Isaya 35:5, 6; Yeremia 33:6; linganisha Zaburi 103:1-5.) Baada ya kusamehewa dhambi zao za awali, Wayahudi wanaorudi wataanzisha tena ibada safi huko Yerusalemu.

      21. Waabudu wa Yehova leo hupata uponyaji wa kiroho kwa njia zipi?

      21 Hata hivyo, unabii wa Isaya unatimizwa leo pia. Watu wa Yehova leo pia wameponywa kiroho. Wamekombolewa kutoka katika mafundisho yasiyo ya kweli kama vile kutokufa kwa nafsi, Utatu, na moto wa mateso. Wao hupata mwelekezo wa kiadili, unaowaweka huru kutoka kwa mazoea ya ukosefu wa adili na kuwasaidia kufanya maamuzi yanayofaa. Na kwa sababu ya dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo, wao wana msimamo safi mbele za Mungu na wana dhamiri safi. (Wakolosai 1:13, 14; 1 Petro 2:24; 1 Yohana 4:10) Uponyaji huo wa kiroho una faida za kimwili. Kwa kielelezo, kuepuka ngono ya ukosefu wa adili na utumizi wa bidhaa za tumbaku huwalinda Wakristo dhidi ya maradhi ya kuambukizwa kingono na aina fulani za kansa.—1 Wakorintho 6:18; 2 Wakorintho 7:1.

      22, 23. (a) Andiko la Isaya 33:24 litapata utimizo gani mkubwa wakati ujao? (b) Waabudu wa kweli leo wameazimia kufanya nini?

      22 Zaidi ya hayo, maneno ya Isaya 33:24 yatatimizwa kwa njia kubwa zaidi baada ya Har–Magedoni, katika ulimwengu mpya wa Mungu. Chini ya utawala wa Ufalme wa Kimesiya, wanadamu wataponywa kimwili na kiroho. (Ufunuo 21:3, 4) Muda mfupi baada kuharibiwa kwa mfumo wa mambo wa Shetani, hapana shaka miujiza kama ile ambayo Yesu alifanya akiwa duniani itafanyika duniani kote. Vipofu wataona, viziwi watasikia, vilema watatembea! (Isaya 35:5, 6) Hiyo itawawezesha watakaookoka wa dhiki kubwa washiriki katika kazi tukufu ya kuigeuza dunia kuwa katika hali ya kiparadiso.

      23 Baadaye, ufufuo utakapoanza, yaonekana wale wanaorudi kwenye uhai watainuliwa wakiwa na afya njema. Lakini dhabihu ya fidia itakapoendelea kutumiwa zaidi, faida nyingi zaidi za kimwili zitatokea, hadi wanadamu watakapofikia ukamilifu. Ndipo waadilifu ‘watakapokuja kwenye uhai’ kwa ukamili. (Ufunuo 20:5, 6) Wakati huo, kwa njia ya kiroho na pia ya kimwili, “Hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” Hiyo ni ahadi nzuri kama nini! Waabudu wote wa kweli leo na waazimie kuwa miongoni mwa wale watakaopata utimizo wake!

  • “Hakuna Mkaaji Atakayesema, Mimi Mgonjwa”
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 354]

      Katika ulimwengu mpya, kutakuwapo uponyaji mkubwa wa kimwili

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki