-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kweli kweli, lile badiliko kubwa lililoanza katika 1914 lilikuwa na matokeo makubwa sana hivi kwamba falme nyingi zilizokuwa zimesimama kwa muda mrefu zilitoweka. Lile angusho la utawala wa zari katika pinduzi la Bolsheviki la 1917 liliongoza kwenye mkabiliano wa muda mrefu kati ya Umarksizimu na ukapitalisti (ubepari). Mitetemo ya badiliko la kisiasa yaendelea kusumbua jamii ya kibinadamu duniani pote. Leo, serikali nyingi zinashindwa kuendelea kwa muda unaozidi mwaka mmoja au miwili. Ukosefu wa imara katika ulimwengu wa kisiasa unatolewa kielezi na kisa cha Italia, ambayo ilikuwa na serikali mpya 47 katika muda wa miaka 42 tu kufuatia Vita ya Ulimwengu 2. Lakini mitetemo hiyo ni utangulizi tu wa badiliko kubwa la kiserikali lenye kufikia upeo mkuu. Tokeo litakuwa nini? Ufalme wa Mungu utachukua utawala kamili wa dunia.—Isaya 9:6, 7.
6. (a) H. G. Wells alielezaje habari ya muhula mpya wenye maana kubwa? (b) Mwanafalsafa mmoja na waziri wa serikali mmoja waliandika nini juu ya muhula wa tangu 1914?
6 Wanahistoria, wanafalsafa, na viongozi wa kisiasa wameelekeza kwenye mwaka 1914 kuwa mwanzo wa muhula mpya na wenye maana kubwa. Miaka 17 ya kuingia katika muhula huo, mwanahistoria H. G. Wells alitoa elezo hili: “Kwa mteremo nabii angetoa unabii wa vitu vizuri. Lakini wajibu wake ni kusimulia anachoona. Yeye anaona ulimwengu ambao ungali unadhibitiwa kiimara na askari-jeshi, wazalendo, wala-riba, na mabarakala wa kifedha; ulimwengu uliojikabidhi kwenye shuku na chuki, ukipoteza kwa haraka sana mauhuru ya faragha yaliyobaki, ukijongeza ki-upofu-upofu kuelekea mapambano makali ya kitabaka, na kutayarisha kwa ajili ya vita vipya.” Katika 1953 mwanafalsafa Bertrand Russell aliandika: “Tangu 1914, kila mtu anayejua maelekeo yaliyo katika ulimwengu amesumbuliwa sana na ule ambao umeonekana kuwa kama mwendo wenye tukio baya na uliokusudiwa kimbele kuelekea msiba unaozidi kuwa mkubwa. . . . Wao wanaona jamii ya kibinadamu, kama shujaa wa hadithi yenye misiba ya Kigiriki, akiendeshwa na miungu wenye kasirani na yeye siye bwana-mkubwa tena wa tukio baya.” Katika 1980 waziri wa serikali Harold Macmillan, akirudisha fikira nyuma kwenye mwanzo wenye amani wa karne ya 20, alisema: “Kila kitu kingezidi kuwa bora na bora. Huu ndio ulimwengu nilimozaliwa mimi. . . . Ghafula, asubuhi moja katika 1914 kitu kizima chote kilikuja kwenye mwisho.”
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 106]
1914—Kigeukio cha Historia
Kile Kitabu Politikens Verdenshistorie—Historiens Magt og Mening kilichotangazwa 1987 katika Copenhagen, kinatoa oneleo hili kwenye ukurasa 40:
“Imani ya karne ya 19 katika mwendeleo ilipata pigo layo lenye kufisha katika 1914. Ule mwaka uliotangulia mfyatuko wa vita, mwanahistoria na mwanasiasa Mdanishi Peter Munch aliandika akiwa na matumaini mazuri hivi: ‘Ithibati yote iko dhidi ya uwezekano wa kutokea kwa vita kati ya serikali kubwa-kubwa za Ulaya. “Ile hatari ya vita” pia itatoweka katika wakati ujao, kama vile imefanya wakati kwa wakati tangu 1871.’
“Kwa kutofautisha, sisi tunasoma katika kumbukumbu zake za baadaye: ‘Ule mfyatuko wa vita katika 1914 ndio kigeukio kikubwa cha historia ya binadamu. Kutoka katika wakati maalumu ulio mwangavu wa maendeleo, ambao katika huo mambo yangefuatiliwa kwa usalama wenye kiasi, sisi tuliingia kizazi cha msiba, hofu kuu, na chuki, kukiwa na utosalama kila mahali. Hakuna yeyote angeweza kusema, na hata leo hakuna anayeweza kusema, kama giza lililoanguka juu yetu wakati huo litamaanisha uharibifu wenye kudumu wa muundo mzima wote wa kitamaduni ambao binadamu amejiumbia mwenyewe kwa mileani zilizopita.’”
-