-
Kelele—Yale Uwezayo Kufanya KuihusuAmkeni!—1997 | Novemba 8
-
-
Matokeo ya Kelele
Kwa kuwa sikio ndilo “kigunduzi bora zaidi” cha kelele, bila shaka ndicho kiungo kielekeacho kuumizwa zaidi na kelele. Madhara kwa chembe za neva zilizo nyetivu za sikio lako la ndani yaweza kutokeza uziwi kabisa. Ni kweli kwamba watu hutofautiana katika kuitikia sauti kubwa. Lakini kuwapo mahali penye sauti zinazozidi decibel 80 hadi 90 kwa kurudia-rudia kwaweza kutokeza uziwi polepole. Kwa kweli, kadiri viwango vya kelele vilivyo juu, ndivyo uwavyo na wakati mchache zaidi ulio salama wa kuwa katika mazingira hayo kabla hujapatwa na madhara ya kusikia.
Gazeti New Scientist huripoti kuwa vinanda vingi vya kibinafsi vinavyouzwa huko Ufaransa vyaweza kutoa kufikia decibel 113. Likitaja uchunguzi mmoja, gazeti hilo lilionelea kwamba “muziki wa roki ukichezwa kwa sauti ya juu zaidi kwa muda wa saa moja katika mashini za kuchezea diski songamano za kibinafsi mara nyingi zilipita decibel 100 na kufikia vilele vya karibu decibel 127.” Tokeo lililo baya hata zaidi ni la kelele inayofanyizwa katika maonyesho ya muziki ambapo wachezaji na wahudhuriaji wako pamoja. Mchunguzi mmoja alipata watu wakiwa wamerundamana karibu na vikuza-sauti vilivyokuwa vimerundikwa kimoja juu ya kingine wakiwa katika hali ya kuzubaa. “Nilikuwa sioni vizuri, mwili wangu ukivuma kwa mdundo mzito wa besi,” asimulia, “na kelele hiyo ilifanya masikio yangu yaniume.”
Kelele yaweza kuwa na matokeo gani kwako? Mamlaka moja yataarifu: “Kelele za daima za kiasi hadi viwango vya juu husababisha mkazo, uchovu, na kuudhika.” “Kuteswa-teswa na kelele hakumfanyi mtu awe bila furaha tu, bali kwaweza kumfanya mtu awe mnyong’onyevu kimwili na kihisia-moyo,” aonelea Profesa Gerald Fleischer, wa Chuo Kikuu cha Giessen, Ujerumani. Kulingana na Profesa Makis Tsapogas, wakati kelele inapokuwa chanzo kikuu cha mkazo, yaweza kusababisha mshuko wa moyo na pia magonjwa mengine ya viungo.
Kukaa mahali palipo na kelele kwa muda mrefu kwaweza kuathiri utu wako. Wakati watafiti wa serikali ya Uingereza walipowauliza wahasiriwa wa kelele walivyohisi kuhusu wale waliosababisha uchafuzi wa kelele, wahasiriwa hao walisema kuwa walihisi chuki, kulipiza kisasi, na hata kuwaua kimakusudi. Kwa upande ule mwingine, wanaofanya kelele mara nyingi huwa wenye kuchokozeka wanapokuwa shabaha ya malalamiko ya kurudia-rudia. “Kelele hupunguzia watu tabia ya kufikiria wengine kuliko wao wenyewe na hutokeza uchokozi na uhasama,” adai mfanya-kampeni mmoja dhidi ya kelele.
Wengi ambao wameteseka kutokana na uchafuzi wa kelele wanatambua kuwa wanapoteza polepole uwezo wao wa kukinza usumbufu. Wao wana maoni kama ya mwanamke mmoja ambaye majirani wake wenye kelele walikuwa wakicheza muziki kwa sauti ya juu kila wakati: “Unapolazimishwa kusikiliza jambo usilotaka kusikiza, hilo lakufanya uwe mnyong’onyevu. . . . Hata wakati kelele ilipoisha, tulikuwa tukiingojea ianze tena.”
-
-
Kelele—Yale Uwezayo Kufanya KuihusuAmkeni!—1997 | Novemba 8
-
-
Kelele na Wewe
“Kelele ndiyo hatari iliyoenea sana ya kiviwanda katika Uingereza leo,” lataarifu gazeti The Times, “na uziwi ndilo tokeo lake la kawaida.” Uchunguzi fulani wa afya na utendaji huonyesha kuwa kelele iliyozidi decibel 85 yaweza kukidhuru kijusu. Uwezo wa mtoto mchanga wa kusikia waharibika, na mtoto mchanga aweza kuwa na mvurugo wa kihomoni na pia kasoro za kuzaliwa.
Kuwa mahali penye kelele ya juu huifinya mishipa ya damu na kupunguza mzunguko wa damu katika viungo vyako. Likiwa tokeo, mwili wako waitikia kwa kutoa homoni ambazo huzidisha msongo wa damu na kuongeza mpigo wa moyo, wakati mwingine hilo likileta mpigo wako wa moyo wa kasi au hata ugonjwa wa angina.
Kelele inapovuruga utaratibu wako, matatizo mengine yaweza kutokea. Usingizi usiotosha waweza kuathiri utendaji wako wa wakati wa mchana. Huenda kelele isibadili mwendo wako wa kazi kwa ujumla, lakini yaweza kuhusika katika idadi ya makosa unayofanya.
-