Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Norway
    2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • MBEGU YA UFALME YAZAA MATUNDA

      Ingawa watu fulani walipendezwa na ujumbe wake, Knud hakukaa sana Skien, jiji la nyumbani. Alilazimika kurudi kwa familia yao nchini Marekani. Hata hivyo, mnamo 1899, alirudi tena Norway baada ya kuombwa na Charles T. Russell aliyekuwa msimamizi wa kazi ya Wanafunzi wa Biblia wakati huo. Ndugu Russell alitaka Knud aanzishe kutaniko nchini Norway. Knud alibeba nakala kadhaa za mabuku mawili ya kwanza ya vitabu Millennial Dawn (baadaye viliitwa Studies in the Scriptures), ambayo yalikuwa yametafsiriwa katika mchanganyiko wa Kinorway na Kidenishi. (Wakati huo, maandishi ya Kinorway yalifanana na ya Kidenishi, na machapisho yangeweza kusomwa nchini Denmark na Norway.) Knud aliwahubiria watu wengi na kuwaachia vitabu, lakini baada ya muda alilazimika kurudi Marekani tena.

      Mwaka uliofuata, Ingebret Andersen, ambaye aliishi karibu na jiji la Skien, alipata kitabu The Plan of the Ages, ambacho huenda kilikuwa mojawapo ya nakala ambazo Knud alileta Norway. Kwa muda mrefu, Ingebret alipendezwa na habari kuhusu kuja kwa Kristo kwa “mara ya pili,” na sasa yeye na mke wake Berthe, walivutiwa na mambo waliyosoma. Punde si punde, Ingebret akaanza kuhubiri. Hata alienda kwenye mikutano ya kidini ili kuwaambia watu kuhusu Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo. Baadaye, aliwatembelea watu waliopendezwa, na muda si muda kukawa na kutaniko la angalau Wanafunzi wa Biblia kumi jijini Skien.

      Knud alipoambiwa na mtu wa ukoo kuhusu kutaniko hilo dogo jijini Skien, alirudi Norway mwaka wa 1904 kumtafuta Ingebret. Alisimama barabarani na kumuuliza mwanamume fulani, “Je, unamfahamu Ingebret Andersen?” Mwanamume huyo akajibu, “Ndiyo, ni mimi.” Knud alisisimka sana hivi kwamba alifungua mkoba wake papo hapo katikati ya barabara, na akaanza kumwonyesha Ingebret vitabu alivyokuwa navyo. Ingebret naye alifurahi kukutana na Knud na kuona machapisho hayo mengi.

      Knud aliwaambia kwa shauku waamini wenzake wa Norway kuhusu tengenezo na kazi ya kuhubiri. Kufikia wakati aliporudi kwa familia yake, ambayo kwa sasa waliishi Kanada, kutaniko la Skien lilikuwa limetiwa moyo sana kusonga mbele.

  • Norway
    2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 92]

      Kutaniko la Skien mwaka wa 1911, pamoja na Ingebret na Berthe Andersen

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki